masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Sunday, June 8, 2014

LEMA: WIZI WA FEDHA ZA IPTL YUMO MBUNGE WA UPINZANI




MBUNGE wa Arusha mjini Godbless Lema amesema miongoni mwa wezi wa fedha za kampuni ya kufua umeme IPTL yumo mbunge wa chama cha upinzani.

Lema alisema hayo jana alipokuwa akiwahutubia wakazi wa Kata ya Miyomboni – Kitanzini uliofanyika katika uwanja wa mnada (well fair) katika Manispaa ya Iringa.



Alisema magerezani wamejaa masikini wasio na hatia huku wezi wakubwa wanaoifilisi nchi wakiwa ni wabunge na mawaziri ambao hawaguswi na kuachwa kuendelea kula raha bungeni.

Alifafanua kuwa akiwa na mwenzake Mbunge Peter Msigwa, wametajiwa mbunge wa chama cha upinzani ambaye alisaini fedha hizo kwa ajili ya matumizi yake binafsi japo kuwa hakumtaja kwa jina na kwamba wanasubiri waziri mwenye dhamana aliweke wazi bungeni ili aweze kushughulikiwa kama ambavyo mbunge yeyote anashughulikiwa akiwa na tuhuma na makosa mbalimbali.

Alisema nchi inatia aibu kugeuka ombamba huku ikiwa na rasilimali nyingi za kila aina ambazo zinawafaidisha wachache wasiona uchungu na nchi wanaoiba na kulindwa kama dhahabu kana kwamaba ni watu muhimu huku masikini wakibambikwa kesi za ajabu ajabu.

“Ndugu zangu, tunapopambana na CCM, tunapambana na wezi, majambazi, mafisadi na wahuni. Unapokuwa na chama kinachouza ndovu, madini, misitu, na ardhi, uhusiano wao na shetani ni wa karibu.

“Unapokuwa na chama kinachotoa sukari kiwandani kwa shilingi 1,000/= na kutoza kodi hadi kufikia 2,000/= au ukiwa na chama ambacho sementi kiwandani inatengenezwa kwa shilingi 4,000/= na kutoza kodi hadi kufikia shilingi 15,000/= ni chama cha mauaji” alisema Lema.

Pia alisema wapo wanasiasa ambao wamefirisika kimawazo na kutumia imani za kidini kuwagawa watangania jambo ambalo wananchi wanatakiwa kuwapuuza wanasiasa wa namna hiyo kwani hawana mawazo ya maendeleo.

“Anayewatenganisha kwa udini ni muhuni tena hapaswi kusikilizwa kabisa. Jaribuni kuwahoji wanasiasa wa namna hiyo kuwa kwani bungeni kuna kukusanya sadaka? Au bungeni kuna kufungisha ndoa? Bungeni ndugu zangu ni kujenga hoja tu wala hakuna sadaka wala kufungisha ndoa” alisema Lema.

Mbunge wa Iringa mjini Mch. Peter Msigwa alisema ikiwa nchi yenye rasilimali nyingi kama Tanzania inategemea asilimia 40 ya bajeti nzima kutoka kwa wahisani na wafadhiri mbalimbali, nchi haina viongozi wenye uwezo wa kufiki jinsi ya kujitegemea.

Alisema cha kushangaza kuna wabunge ambao wapo madarakani kwa miaka mingi lakini majimbo yao hayana maendeleo kwa muda mrefu lakini kazi yao ni kuunga mkono bajeti hewa.

“Mipango yote inaandaliwa kwa ajili ya matajiri na makampuni makubwa yanayokweta kulipa kodi pamoja na kuiba rasilimali za umma au kuwaibia watanzania” alisema.

Alisema inapoonekana mmoja anaonewa jamii inapaswa kupiga kelele kwa kuwa kuonewa kwa mtu mmoja ni kuonewa kwa jamii nzimaa.

“Akionewa machinga, nesi hapaswi kukaa kimya, akionewa mwalimu machinga hapaswi kukaa kimya. Watu wote tunategemeana kwa kazi tunazozifanya” alisema.

Naye John Mwambigija maarufu kwa jina la Mzee wa upako amewataka wananchi wa Mkoa wa Iringa wasivunjike moyo na uchaguzi wa Kalenga bali uwe changamoto kwa chaguzi zijazo na kujipanga kwa ajili ya kukabiliana nazo.

“Kazi ya mabadiliko siyo rahisi lakini cha msingi tunatakiwa kuungana kwa pamoja ili tuwe na nguvu ya pamoja.

“Umasikini tulionao unasababishwa na mawazo mepesi walio nayo viongozi wasio na uwezo wanaotumia nafasi zao kutuhujumu” alisema Mwambigija.

No comments:

Post a Comment