masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, June 10, 2014

MBUNGE MSIGWA AVIJIA JUU VYOMBO VYA HABARI MKOANI IRINGA

Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA) amevijia juu baadhi ya vyombo vya habari mkoani humo kutokana na kile alicho kiita ni kutumika vibaya na baadhi ya wanasiasa wasiyo na mapemzi mema na wananchi wa jimbo hilo.

Akizungumza katika mkutano wake na wananchi wa kata ya Ruaha  juzi, Msigwa ambaye pia ni waziri kivuli wa mali asili na utalii alivitaja kwa majina vyombo hivyo (majina  tunayo) aliwataka wananchi hao kuto viamini  vyombo hivyo na kwamba vimekuwa vikitumika vibaya na chama tawala chama cha mapinduzi (CCM).

Katika kuonesha kwamba anavifahamu vizuri vyombo hivyo pamoja na  waandishi wao (siyo wa mtandao huu) Msigwa alisema baadhi yao wamekuwa wakishiriki katika kampeni za chini kwa chini za chama cha mapinduzi ikiwemo kuwarubuni vijana kwa fedha  huku wengine wakishiriki katika mafunzo ya ulinzi  kwa vijana wa CCM maarufu kwa jina la green gurd yanayoendelea kufanyika katika kambi ya Ihemi mkoani Iringa.

Msigwa alisema watanzania wanatakiwa kukumbuka vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyowahi kutokea nchini Rwanda kwamba kisa kilikuwa ni vyombo vya habari ambavyo vilishindwa kutumia ipasavyo taaluma yao na hatimaye kuliingiza taifa la Rwanda katika mapigano makubwa na ya kihistoria.

“Baadhi yenu waandishi na watangazaji wa radio hapa mkoani mnatumika vibaya, nawaaambieni mtaiingiza nchi hii  katika vita  kubwa. Mimi niliaminiwa na wananchi wa jimbo la Iringa sikupita kwa ngekewa kama mnavyosema waheshimu hawa walionichagua ” alisema.

Katika hatua nyingine mbunge Msigwa amewaonya baadhi ya waandishi hao kwa  kuukejeli ubunge wake mbele ya wananchi kwa kumwita mbunge aliyechaguliwa kwa ngekewa na kwamba kitendo cha waandishi hao kugeuza vyombo vyao vya habari kuwa jukwaa la siasa hata weza kulivumilia kamwe.

Siku za hivi karibuni mbunge huyo amekuwa akisikika akilalamikia vyombo hivyo vya habari kushindwa kumtendea haki yeye pamoja na wananchi wa jimbo hilo kwa kushindwa kuandika ukweli wajinsi  utekelezaji wa ahadi zake ambazo aliahidi katika kipindi cha kampeni za uchaguzi zilizopita mwaka 2010 jambo ambalo alisema linalenga kumgombanisha  na wapiga kura wake.

Aidha Msigwa alisema baadhi ya waandhishi hao wamethubutu kuwarubuni wananchi kwa kuwaambia kuwa msaada wake wa vitanda vya wagonjwa ambavyo alivitoa mapema mwaka jana na kukabidhi uongozi wa hospitali ya Wilaya iliyopo Frelimo  haukukidhi haja kutokana na vitanda hivyo kuonekana kuwa na madhara kwa wagonjwa jambo ambalo mtandao huu umefanya utafiti na kuthibitisha kuwa  vitanda vinatumika na wananchi wanaotumia hospitali hiyo bila madhara yoyote.

Akizungumza na mtandao huu hospitalini hapo, daktari ambaye aliomba jina lake lisiandikwe alisema hakuna madhara yaliyotokea kwa mtu yoyote kutokana na vitanda hivyo na kwamba uvumi wa kuwapo na madhara kwa vitanda hivyo si wa kweli.

“Vitanda vilivyopo vinaendelea kutumika bila tatizo japo kuwa nimesikia kuna baadhi watu wakisema kuwa vina madhara. Sisi wahudumu tuliopo hapa hatujawahi kuyaona madhara yoyote na tunawaambia wananchi kuwa hakuna tatizo ambalo inatokana na vitanda. Hayo ni maneno ya watu wasiopenda maendeleo.

“Nawaombeni wanasiasa msiingilie taaluma za watu. Msijinadi kwa kutumia uongo kuharibu taaluma za watu. Watu wanaotangaza uongo wanamna hiyo siwapendi kwa sababu sisi tunataka huduma yetu iwe nzuri na ya kuheshimika. Isitoshe wanaotangaa uongo huo si wale walioleta vita. Mimi nasema kama Mbunge angeweza, alete vitanda vingine kama hivi kwa sababu vitanda vina hadhi” kilisema chanzo chetu.

Malalamiko ya Mbunge huyo yanakuja kipindi ambacho chama cha mapinduzi kinapigana kufa na kupona kutaka kulipokonya jimbo hilo ambalo wananchi wa Iringa mjini mwaka 2010 waliamua kwa mapenzi yao kumchagua Msigwa kama mwakilishi wao halali bungeni.

Hata hivyo Mch. Msigwa pamoja na kuwataka wananchi kuwapuuza waandishi hao lakini pia ameendelea kuungwa mkono na akina mama, wasomi, wazee pamoja na kundi la vijana katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya jimbo lake la Iringa mjini.

Miongoni mwa ahadi ambazo mbunge Msigwa aliahidi na tayari amekwisha onesha uwezo wa kuzitekeleza ni pamoja na kuwajengea wananchi uwezo wa kujitambua na kutambua haki zao, kuboresha miundo mbinu ya barabara ambazo zinaendelea kutengenezwa, pia aliahidi  kuwasha taa za baadhi ya barabara za mitaa ya  mji wa Iringa zikiwamo za stendi kuu ahadi ambayo imetekelezwa.

Pamoja na hayo Msigwa katika kipindi cha kampeni aliahidi kutoendeleza utamaduni uliokuwa umejengeka kwa wananchi wa jimbo hilo wa kupewa fedha kutoka kwa wabunge waliopita na kwamba yeye atawajibika kuwajengea uwezo katika kutafuta riziki kuliko kuwategemezi .

Ahadi nyingine ambayo inakumbukwa sana na wapiga kura wake ni ile ya kumwajili mwanasheria ambaye anajukumu la kuwasimamia wananchi katika kutafuta na kudai haki zao pindi wapatapo matatizo yanayohusu utashi wa kisheria jambo ambalo pia amelitekeleza.

Msigwa pia aliahidi kukomesha tatizo la ukosefu wa maji ambapo hadi sasa jimbo la Iringa mjini linapata maji kwa asilimia tisini jambo ambalo wananchi wa jimbo hilo wanajivunia ukilinganisha na majimbo mengine kama Kilolo, Mufindi kaskazini, Isimani pamoja na Kalenga ambayo yote kwa pamoja yanaongozwa na wabunge wa chama cha mapinduzi lakini upatikanani wa maji ni wa tabu.

Hata hivyo katika kuonesha nia yake ya kweli aliyowahi kuahidi katika majukwaa ya kampeni za  uchaguzi uliopita mbunge  Msigwa ndiye mbunge pekee  kuwahi kutokea kupitia chama pinzani  nchini na ambaye amekuwa kivutio kwa wengi ndani na nje ya bunge hasa katika michango yake awapo bungeni.

No comments:

Post a Comment