HALI ya jengo la shule
ya Sekondari ya Kata ya Kimala Wilaya ya Kilolo katika Mkoa wa Iringa inazidi
kuwa tete kutokana na jengo hilo kudaiwa kujengwa chini ya kiwango na kubomoka
huku likiwa linaendelea kujengwa.
Hali hii imewalazimu
wananchi kuwabana viongozi wa kata hiyo akiwemo diwani na ofisa mtendaji ili waweze
kutolea maelezo jambo hilo.
Diwani huyo Mejus
Mgeveke (CCM) pamoja na Ofisa Mtendaji wa Kata hiyo Deus Wambura wamekataa wito
wa wananchi wa Kata hiyo waliowataka kufika kwenye Kikao cha Halmashauri ya
Vijiji kilichopangwa kufanyikaia katika Kijiji cha Idunda ili kutolea maelezo
juu ya ujenzi wa shule ya sekondari ya Kata hiyo unaosuasua na jengo kuendelea
kubomoka huku ujenzi ukiwa haujakamilika.
Viongozi hao wamefikia
uamuzi huo baada ya wananchi kuzitaka halmashauri za vijiji vyao kukutana na
uongozi wa Kata kujadili na kuwarudishia majibu ya kwa nini jengo la shule hiyo
kuzidi kubomoka huku ujenzi ukiendelea licha ya wananchi hao kuendelea kutoa
michango huku viongozi wakishindwa kuwasomea wananchi mapato na matumizi miaka
yote.
Kwa mujibu wa barua
hiyo iliyoandikwa 19 Mei 2014 iliwataka viongozi hao kuhudhuria kikao hicho
kilichotarajiwa kufanyika 22 Mei 2014 na kwamba baada ya kikao hicho
kingefuatwa na mkutano wa hadhara ili kutoa majibu kwa wananchi.
Wito huo ulikuja baada
ya wananchi wa Kata hiyo kuwataka viongozi wa vijiji vyao kutoa majibu
yakuridhisha kutokana na maendeleo ya ujenzi wa shule huku wakihoji ni
kinachokwamisha kuwasome amapato na matumizi ya jenzi huo tangu mwanzo.
Kutokana na wito huo
ofisa Mtendaji wa Kata hiyo Deus Wambura aliandika barua kukataa kuitika wito
huo huku akieleza kuwa ofisi yake haiwajibiki kusoma mapato na matumizi kama
wananchi wanavyodai.
Mtandao huu umefanikiwa kupata nakala ya barua iliyoandikwa na Wambura ofisa mtendaji wa
kata Mei 19 mwaka huu siku hiyo hiyo baada ya kupokea barua ya wito iliyokiri
kuwa ofisi yake haiwajibiki kutoa taarifa ya mapato na matumizi.
“Sambamba na hilo,
ilishaelezwa kwamba siyo wajibu wa ofisi ya kata kuzunguka katika vijiji kusoma
mapato na matumizi badala yake yatasomwa kwenye vikao vya W.D.C baada ya hapo vijiji
vitaenda kusoma kwa wananchi” imeandikwa kwenye barua hiyo.
Katika hatua nyingine
wananchi wametaka ujenzi huo usimame haraka hadi hapo watakapopatiwa taarifa za
mapato na matumizi kwa maelezo kuwa ujenzi huo unawaumiza wananchi na
kuwatajirisha watu wachache akiwemo diwani wa Kata hiyo.
Jumla ya wajumbe 17 wa
kijiji cha Idunda wametia saini wakiwaunga mkono wenzao wa kijiji cha Kimala
kutaka ujenzi wa shule hiyo usimame hadi pale yatakapopatikana na majibu ya
kuridhisha.
Wananchi wametoa
masikitiko yao kuwa diwani huyo pamoja na ofisa mtendaji wa Kata hiyo wmekuwa
wakitumia taarifa za uongo kwa wananchi wanapotaka kuhujumu mali za wananchi.
“Cha kushangaza diwani
kwa kushirikiana na afisa mtendaji wa Kata wamekuwa wakitutangazia kuwa kuna
ndege itapita usiku wa manane kupima ardhi kwa wananchi tusitoke nje kumbe ndio
njia wanayoitumia kuiba sementi na vifaa vya ujenzi ili wasionekane.
Wakitangaza hivyo mgambop wamekuwa wakitembea usiku kuangalia watu wanaokuw
macho ili wakamatwe kwa ajili ya kuwalipisha faini.
“Ni mara ya pili sasa
tunadanganywa, mara ya kwanza walisema ndege itapita usiku kupima ardhi na mara
ya pili walisema ndege itapita usiku kumwaga hewa chafu na kuwataka wananchi
wasitoke nje wasije wakadhurika kumbe ndio wakati wao wakufanya hujuma” vyanzo
vyetu vimeeleza.
Wananchi wa kata hiyo
wanapanga kuandamana hadi ofisi za Wilaya kupata majibu ya michango yao inakokwenda
ili kupata ukweli halisi wa nguvu zao zinakoishia.
Hata hivyo viongozi wa
kijiji cha Kimala, Sadrus Lwanzali mwenyekiti wa kijiji na Festo Mtenga ofisa
mtendaji wa kijiji wameelezwa kuwa hawana msaada wowote kwa wananchi kutokana
na kumezwa na diwana na ofisa mtendaji wa kata.
“Diwani akiwa na
mtendaji wa kata wanatumia mabavu kwa sababu hata viongozi wa vijiji hawana
sauti yoyote. Viongozi wa vijiji ni kama wamenunuliwa maana tukiwaagiza
hawatuletei majibu yakueleweka” vyanzo vyetu vinaeleza.
Mwishoni mwa mwaka jana mtandao huu uliripoti juu ya jengo la shule hiyo linavyobomoka huku
likiendelea kujengwa huku wananchi wakilalamika kutosomewa mapato na matumizi
tangu mwanzo wa ujenzi.
Hali ya jengo hilo
inazidi kuwa mbaya na kusababisha wananchi kugoma kutoa michango yao kwa maelezo
kuwa haiwanufaishi n badala yake inamnufaisha diwani na familia yake badala ya
kufanyia kazi inayokusudiwa.
Viongozi hao wanahaha
kufanya utaratibu wa kuziba nyufa zinazopasuka katika jengo hilo ambazo
zinaonesha hatari ya jengo hilo kuanguka wakati wowote kutokana natatizo
linalozidi kujitokeza.
Utafiti wa gazeti hili
umebaini kuwa mjenzi wa jango la shule hiyo ni mtwasi wa diwani huyo kwa maana
ya kuwa wameolea nyumba moja jambo lililochangia kupeana tenda kirafiki ili
diwani huyo awe na maamuzi yake kirahisi.
Awali waliziba nyufa
zilizokuwa zimepasuka lakini kutokana na kile kinachodaiwa jengi kujengwa chini
ya kiwango, jengo hilo linazidi kudhoofika siku hadi siku.
No comments:
Post a Comment