| Mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa akihubiri kanisani wakati wa maadhimisho ya Mika katika Seminari ya Mafinga. |
| Mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa akiwa pamoja na Mapadre na wanafunzi wa kidato cha sita wanaohitimu nje ya Kanisa mara baada ya Misa Takatifu. |
| Mhashamu askofu Ngalalekumtwa akikabidhi cheti cha mmoja wa wahitimu wa kidato cha sita ukumbini. |
| Mhashamu askofu Ngalalekumtwa akihutubia wanafunzi na wageni waalikwa katika ukumbi wa Seminari ya Mafinga wakati wa mahafali. |
RAIS wa Baraza la Maaskofu
Katoliki Tanzania (TEC) Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa amewataka Wakristo
nchini kuwa na hamu ya kumjua Mungu ili kustawisha Imani na kuishi katika
mshikamano wa amani na upendo.
Askofu Ngalalekumtwa
ameyazungumza hayo wakati wa maadhimisho ya Misa Takatifu iliyofanyika katika
Seminari ya Mafinga katika Jmbo la Iringa na kusema kwamba kumjua Mungu ni kuishi
katika uadilifu na uaminifu.
Amesema kazi ya kumtafuta Mungu
ni wanadamu bali si Mungu kumtafuta mwanadamu kwani mwanadamu ameumbwa na
kupewa akili na utashi wa kuweza kupambanua mambo mengi na kuchukua hatua ya
maisha yanayompendeza Mungu au kuishi kadiri yeye atakavyo kwa maamuzi yake
binafsi.
“Wakati tunaendelea kusherehekea
Sikuu Kuu hizi za Pasaka tuwe na hamu ya kumjua Yesu Kama Tomaso alivyofanya.
Imani ya Kipasaka ni ile inayoangazwa na Mungu Baba na Mwana na Kristo si wa
kukimbizana naye bali ni wa kumkimbilia” amesema.
Amesema mwanadamu akiishi kwa
haki atakuwa anatimiza maagizo ya Mungu anayetaka watu waishi bila
kubughudhiana, waishi kwa upendo na kuacha chuki kwa kila mmoja.
Askofu Ngalalekumtwa ambaye pia ni askofu wa Jimbo la Iringa amesema uadilifu wa mtu
humfanya kuheshimika na wengine na kwamba ndiyo njia ya kuufikia Utakatifu
ambao Mungu anapenda wanaomtumainia waufikie.
“Uadilifu ni tunda ambalo
tunalihitaji katika maisha yetu. Haki na uadilifu, haki na uaminifu ni tunda
muhimu kwa wanadamu wanaompenda Mungu. Tunapaswa huishi kama viumbe wenye
hekima” amesema.
Hata hivyo amesema Kanisa ndicho
chombo cha kuandaa raia wa mbinguni ambao wanafundishwa kuishi kwa nidhamu
wakiongozwa na kiongozi Mkuu Yesu Kristo.
Amesema kila mmoja anapaswa
kumshika mwenzake katika umoja ambapo kila mmoja anayo mbegu ya utakatifu
ambayo anatapaswa kupanda katika mioyo yaw engine kusudi waweze kuambukizwa
utakatifu na hatimaye waweze kufuata maisha yanayompendeza Mungu na wanadamu
hapa duniani na kuwa wanafunzi wazuri wa Yesu Kristo.
“Hakuna mnyonge ndani ya Kanisa
kwani haki ni zile zile. Kuweni na utu na ubinadamu. Wote sisi ni watarajiwa wa
mji wa mbinguni, kila mmoja ni mtakatifu mtarajiwa ila cha muhimu ni kuishi kwa
haki. Tunaichezea huruma ya Mungu bila sababu.
“Waakatifu Yohane wa XXIII na Yohane
Paulo wa II ni watu wa kuigwa katika maisha yetu. Katika kutangazwa watakatifu
hawa watumishi wa Mungu, unakumbushwa kuwa ni watu wa amani, upendo, huruma na
tunapaswa kuishi kama viumbe wenye hekima” amesema.
Misa hiyo ilikwenda sambamba na
mahafali ya kidato cha sita ambapo jumla ya wanafunzi 41 waliagwa katika Seminari hiyo.
Akiwakabidhi vyeti wanafunzi hao,
askofu Ngalalekumtwa amewataka kutumia elimu yao katika kuunganisha watu kuishi
maisha ya kupendana na kuepukana na mambo yasiyo na maana ambayo ni chanzo cha
kuvuruga amani na upendo.
Amewataka kuwa viongozi wa mfano
kwa ulimwengu kwa uishi katika maisha yenye kuzingatia haki za binadamu na kuwa
kioo kwa kila wakubwa kwa wadogo.
No comments:
Post a Comment