masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Saturday, May 3, 2014

WAKAZI WA MTAA WASUSA KUFANYA USAFI KATIKA MTAA WAO. > WAWATUHUMU VIONGOZI WAO KUWACHNGISHA FEDHA PASIPO KUFANYA KAZI. > OFISA AFYA KATA AWATUPIA LAWAMA WATENDAJI WA MTAA.

Waandishi wa habari wa Mkoa wa Iringa wakielekea Mtaa wa Ilala kufanya usafi katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani hii leo.
Waandishi wa Habai wa Mkoa wa Iringa wakifanya usafi katika Mtaa wa Ilaa Siku ya maadhimisho ya Uhuru wa vyombo vya Habari duniani.




WAKAZI wa Mtaa wa Ilala katika Manispaa ya Iringa wamesusa kufanya usafi katika mtaa wao kwa kile walichoeleza kuwa wanachangishwa michango kwa ajili ya usafi.

Madai hayo yamekuja baada ya waandishi wa Habari kukusanyika kufanya usafi mtaani humo katika siku ya maadhimisho ya Uhuru wa vyombo vya Habari duniani.

Wakiohijiwa na mtandao huu mtaani humo, wakazi wa mtaa huo wamsema ofisa mtendaji wa mtaa pamoja na ofisa mtendaji wa Kata ya Ilala wamekuwa wakichukua mchango kwa wananchi kwa ajili ya usafi lakini hakuna kinachoendelea.

Wakieeleza kuto kujitokeza kuungana na waandishi wa habai walikua wakifanya usafi katika mtaa wao, wamesema wasingejitokeza kutokana na tabia ya viongozi wao kuwahadaa kuchukua fedha pasipokufanya kazi yoyote.

Alipotakiwa kutaoa ufafanuzi juu ya suala hilo, ofisa afya Kata ya Ilala Gaudence Haule amesema kutokujitokeza kwa wananchi kunatokana na watendaji wa mitaa kutoa taarifa sahihi kwa wananchi juu ya kushiriki usafi katika mtaa wao.

“Taarifa walizopewa wananchi kwa watendaji wao juu ya kushiriki usafi siyo sahihindiyo maana waandishi mnaona wananchi hawana hata mpango wa kushiriki licha ya kuwa mnafanya usafi katika maeneo yao wenyewe.

“Suala la uafi ni la mtu mmoja mmoja kuanzia kwake mwenyewe lakini inapofikia mtu hawajibiki hata sehemu yake mwenyewe usafi wake binafsi unatia shaka. Tusipobadilika hakika itakuwa ngumu hata kwetu wenyewe juu ya afya zetu” amesema.

Wakati huo huo Katibu Mtendaji wa Chama cha waaqndishi wa Habari Mkoa wa Iringa Francis Godwin  amesema licha ya Manispaa ya Iringa kuwa ya pili kwa usafi kitaifa, bado inakabiliwa na changamoto kubwa juu ya usafi kwa ujumla kutoka na wananchi wewenyewe kutokuwa na mwamko wa ufasi.

Amemtaka ofisa usafishaji wa Manispaa kuhakikisha vitendea kazi vinakuwepo kila eneo ili wananhi waweze kuwajibika kufanya usafi ipasavyo badala ya kutupa taka hovyo kila sehemu.

Godwin amesema waandishi  wa Habari Mkoa wa Iringa wameamua kuadhimisha siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari kwa vitendo ili kuuonesha umma vyanzo mbalimbali vya Habari ikiwa ni pamoja na sehemu zao wanazotupa taka.

Pia amesema waandishi wa Habari kufanya usafi, ni kuionesha jamii kuwa mwandishi anawajibika kwa mwananchi katika mambo mbalimbali yanayomzunguka katika maeneo yake.

Ofisa usafishaji wa Manispaa Alon Mafumiko amesema suala la usafi katika Manispaa ya Iringa linakabiliwa na changamoto kubwa ikiwemo ya wananchi kuchoma vifaa vya kuhifadhia taka na kwamba kati mapipa ya taka 50 yaliyokua yamesambazwa na Manispa katika Manispaa nzima kwa ajili ya kubebea taka yamechomwa na wananchi na kubaki mapipa 10 tu.

“Nawaomba wanachi watambue kuwa sehemu bila usafi siyo ustaarabu kwa hiyo kila mmoja awajabike ili tuweke mazingira yetu safi” amesema Mafumiko.

No comments:

Post a Comment