masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Friday, January 3, 2014

WATUMISHI WA MUNGU KUWENI WAAMINIFU: ASKOFU










WATUMISHI wa Mungu wametakiwa kuzingatia maadili yao katika maisha yao yote kwa kuishi kwa tabia njema ili waeze kushiriki kazi ya kulea na kuwalisha wanadamu maneno ya kiroho.

Wamekumbushwa hayo leo na mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa wa Jimbo la Iringa alipokuwa akitoa daraja Takatifu la Ushemasi katika Kanisa Kuu la Kiaskofu Parokia ya Kihesa jimboni humo.

Askofu Ngalalekumtwa ambaye pia ni Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania na msimamizi wa kiti cha kitume Jimbo Kuu la Songea amesema huduma ya shemasi inaambatana na maisha ya useja ambapo wanapaswa kuelekezamiili yao kwa Mungu.

“Mashemasi wanapaswa kuwa na tabia njema ili waweze kuishika siri ya imani katika dhamiri safi. Miili yao, mioyo yao na nafsi yao yote imuelekee Mungu kwa umoja usiogawanyika” amesema.

Amesema mashemasi ni walezi ambao wanapaswa kuwamfano wakuigwa bila kupenda kupita njia za kijanja kwa kujificha bali wanapaswa kufanya kazi zao kwa uwazi.

Amefafanua kuwa huduma ya mashemasisi katika Kanisa Katoliki ni kuwa msaada kwa askofu na Baba Mtakatifu ili waweze kuhudumia altare, kuongoza sala, kusimamia na kubariki ndoa, kuongoza sala, kuongoza ibada ya mazishi na kuwahudumia wanadamu wote kwa upendo.

Pia amesema Mashemasi wanashiriki kutangaza habari njema kwa mataifa ili jamii yote iweze kuishi kwaupendo thabiti na kukemea mambo maovu yanayohatarisha amani ya wanadamu kote duniani kwa kuwa Kristo hupenda amani.

Hata hivyo anawakumbusha kuwa wao ni watunzaji wa siri ya wokovu na watendaji katika kuwapeleka wanadamu kwa Mungu.

“Iweni na moyo wa huruma, upendo kwa watu mnaowahudumia. Tunzeni nafsi zenu ili msilaumiwe mnapohudumia. Kuanzia sasa mtakalokuwa mnalitenda mnalitenda kwa niaba ya Kanisa Katoliki.

“Jitahidini kutenda kwa haki na usafi siyo kwa ujanja ujanja. Kuweni wajumbe wazuri katika kutoa huduma njema. Kuweni naheshima, uaminifu, upendo, nidhamu, utiifu, upole na uadilifu wa Kristo ili mkaitende kazi iliyo haki kwa watu wote” amesema.

Pia amewataka Wakristo kuwaombea watumishi waMungu ili katikahudumazao wapewe nguvu ya kumshinda mwovu shetani na kufanya haki kila wakati.

No comments:

Post a Comment