masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Monday, January 20, 2014

TUNAKARIBIA KUTUA MZIGO: WANANCHI



WANANCHI wa Kata ya Ibumu Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa wamesema wanakaribia kutua mzigo na kupunguza uchovu walionao ambao unasababishwa na utawala dhalimu wa kiimla waliokuwa wakitawaliwa katani humo.

Wameyazungumza hayao jana katika viwanja vya kijiji cha Kilala Kidewakatani humo katika uzinduzi wa kampeni za kumnadi mgombea wa Udiwani kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) July Mpugula.

Mzee ambaye aliongea na gazeti hili pembeni wakati mkutano ukiendelea akiomba jina lake lisiandikwe alisema CCM imeanza kuagwa rasmi kutokana na viongozi wanaopitia chama hicho kuwa ni viongozi wa matumbo na familia zao na kuwafanya wazee kuwa watumwa wao.

“Ndugu yangu anagombea udiwani kupitia CCM lakini hata kwenye mikutano yake siwezi kwenda kwa sababu namfahamu vizuri kuwa akiwa diwani huyo tutalia zaidi ya aliyekuwepo kabla. Kweli nimeamini kuwa CCM wanataka watu wezi kwa sababu ndugu yangu huyu ni mwizi wa kutupa kwenye vijiji vyetu lakini nimeshangaa chama kimemsimamisha kuwa kugombea udiwani. Mimi mwenyewe ni CCM lakini kwa hapa! Haa! Siwezi kumpa kura yangu” kilisema chanzo chetu.

Akimnadi mgombea Katibu wa Chadema Mbeya mjini ambaye pia ni mkufunzi wa Chadema ni msingi Christopher Mwamsiku alisema July amesimamishwa si kwa sababu ya urembo wake bali ni kwa sababu ya uwezo wake na kuwataka wananchi kumuunga mkono ili autumie uwezo wake kusimamia shughuli za maendeleo.

Akiongea kwenye mkutano huo aliwataka Polisi kuacha vitisho kwa wananchi ambao wametulia kwenye mikutano ya Chadema na kwamba chama kinalindwa kwa sababu ya umakini walio nao.

“Angalia sehemu zenye tunu ndizo zinazolindwa kwa mfano angalia Benki zinalindwa, Madini yanalindwa, taasisi za fedha na sehemu nyeti zote zinalindwa. Mikutano ya CCM Polisi hamlindi na badala yake mmeelekeza nguvu kwenye mikutano ya Chadema. Kitu chochote kinacholindwa ndicho cha maana zaidi” alisema.

Naye Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Kilolo Oliani Mkemwa alisema Wilaya ya Kilolo imekuwa shamba la Bibi kutokana na kukosa usimamizi wa watu kutumia fursa hiyo kukwapua fedha za maendeleo.

Alisema tatizo la wizi katika Halmashauri ya Kilolo linatokana na kuwepo kwa madiwani wa chama kimoja cha CCM ambao wote ni wapiga dili na kukosa meno ya usimamizi.

Patrick Ole Sosopi aliesema kwa miaka 50 rasilimia za nchi zimeliwa na watu wachache ambao ni viongozi wa CCM na kuwaacha wananchi wakihangaika bila sababu na kuwataka wananchi kuamka na kutoa adhabu kwa watu wanaoiba rasilimali zao.

Alisema michango imekuwa mingi licha ya wananchi kulipa kodi kila siku kwa sababu ya watu kuwageuza wenzao kuwa chanzo cha kipato cha familia zao.

Mgombea udiwani kupitia Chadema July Mpugula akijinadi alisema wananchi wamekuwa wakipigwa makofi kila upande na viongozi wasio na huruma na kuomba wananchi wamchague ili aende kuwatafuti kinachowapiga makofi.

“Naomba mnitume niende nikawawakilishe kwenye Halmashauri ili niwajulishe nani amekuwa akitupiga makofi kila kunapokucha tunaishi kama wakimbizi kutokana na watu kutufanya watumwa.

“Siendi huko kwa sababu ya kutaka kujinufaisha ila nataka kushirikiana nanyi kuleta maendeleo ambayo watu wameyapeleka majumbani mwao. Wizi wa mali zetu nitahakikisha hakuna anayetuibia kirahisi kama walivyokuwa wanafanya” alisema.

Katika mkutano huo wanachama wa chama cha mapinduzi 46 walirudisha kadi za chama hicho na kujiunga na Chadema huku wanachama wapya 102 wakijiunga na Chadema.

Kampeni za uchaguzi huo zinakuja baada Kata hiyo kuwa wazi kutokana na aliyekuwa diwani wa kata hiyo Jeremiah Ikanyagwa kufariki.

No comments:

Post a Comment