masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Monday, January 27, 2014

KADA WA CCM ANUSURIKA KICHAPO KWENYE MKUTANO WA CHADEMA UKUMBI. ABWAO NA KIKOTI WAMOKOA.

Mgombea udiwani kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Oscar Ndale akiwa kwenye gari akiwapungia wananchi mkono wakati wakitoka kuhani msiba kabla ya kuanza mkutano Ukumbi.

Patrick Ole Sosopi akiwahutubia wananchi wa Ukumbi.

Brian Kikotiakiwahutubia wananchi wa Kata ya Kukumbi jana.

Katibu wa Mbunge wa Ubumbo (Chadema) akiwahutubia wananchi wa Ukumbi.

Mbunge wa viti maalumu Chiku Abwao (Chadema) akiwahutubia wananchi wa Ukumbi jana wakati wa uzinduzi wa kampeni za kumnadi mgombea kupitia chama hicho.

Mbunge wa viti maalum Chiku Abwao kushoto akimnadi mgombea wa udiwani Oscar Ndale kulia na nyuma ni Brian Kikoti wakiwa jukuani.

Mbunge wa viti maalum Chiku Abwao (Chadema) akiwa na viongozi mbalimbali wachama hicho.
Kada wa Chama cha Mapinduzi God Mbilinyi aliyenusurika kichapo kwenye mkutano wa Chadema jana Ukumbi.

Mwananchi mbalimbali wakiwa kwenye mkutano wakimsikilizamgombea wa udiwani wa Chadema katika Kata ya Ukumbi jana.

Wananchi wakiwa wamejitwisha viti wakijikinga mvua wakati wa mkutano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uzinduzi wa kampeni za kumnadi mgombea wa udiwani kupitia chama hicho jana Ukumbi.

Watu mbali mbali wakiwa kwenye mkutano wa Chadema jana katika Kata ya Ukumbi.



UZINDUZI  wa kampeni za kumnadi mgombea wa wa udiwani kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika Kata ya Ukumbi Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa jana ulitaka kuingia dosari baada ya kijana anayeaminika kuwa ni kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Gody Mbilinyi kunusurika kichapo.



Mbilinyi alinusurika kichapo na wananchi waliokuwepo kwenye mkutano huo kwa madai kuwa ametumwa na CCM kuleta fujo hali iliyowalazimu Brian Kikoti na Mbunge wa viti maalum Chiku Abwao kumnusuru kuwa aachwe.



Hali hiyo ilijitokeza wakati Kikoti akiwa jukuani akinadi sera na kumnadi mgombea wa Oscar Ndale pale Mbilinyi alipotokea nyuma ya pale walipokuwa wamekaa viongozi wa Chadema ambapo mayowe yalianza akamatwe huyo huku wakianza kumsogelea jambo lililomlazimu Kikoti na Mbunge Abwao kusimama na kuwataka aachwe.



“Mmwacheni huyo hata kama ametumwa hakuna jambo baya tunalolifanya hapa. Mkutano wetu ni wa amani upo kwa mjibu wa sheria, hatujaja kutukana kama walivyofanya wao jana hapa kuporomosha matusi badala ya kunadi serazao. Sisi tutakuwa wa mwisho kujibu mapigo kwa sababu tupo makini” alisema Kikoti.



Akimuombea kura mgombea wa Chadema alisema CCM wamekuwa ni watu wa ahadi zisizotekelezeka ambapo kila siku wanaeleza ahadi tu na kusahau kuwa walikwisha kuahidi kitu hicho hicho ikashindikana kutekeleza.



“Ukumbi sasa tumechoka kuletewa mamluki. Sasa tunataka kijana mwenye upeo, mwenye uchungu na wanaukumbi wenzake, ambaye anaonja machungu moja kwa moja. Si mtu wa kuja” alisema.



Patrick Ole Sosopi alisema umefika wakati wa kuachana na watu wanaowageuza wenzao kuwa mitaji yao huku maisha yakiwa mabaya kila kukicha.



“Tukiendelea kukubali wanavyotudanganya tutakuwa wajinga. Zaidi ya miaka 50 tumekuwa na maadui watatu maradhi, ujinga na umasikini na sasa ameongezeka adui mwingine ambaye ni rushwa inayosababishwa na CCM.



“Kilolo ina rasilimali nyingi ambazo zinatakiwa kumsaidia kila mmoja lakini badala yake kumekuwa na michango inayokuwa kero kwa wananchi. Hatuhitaji michango inayowabughudhi watu bali tuataka michago inayoleta maendeleo” alisema.



Akimnadi mgombea kupitia Chadema Mbunge wa viti maalum Chiku Abwao (Chadema) alisema mapenzi ya CCM kwa wananchi yamekwisha na kuwataka wanaukumbi kutumia nafasi iliyopo kuikataa.



Alisema ukombozi wa wananchi upo katika uwezo wao na kwamba kitendo cha Ukumbi kuwakatika sura inavyoonekana sasa kwa muda wa zaidi ya miaka 50 ni adhabu.



“Kitendo cha kuwanyima elimu watu wa Kilolo si cha bahati mbaya. Sura mliyo nayo watu wa Kilolo si sura halali. CCM wamewazidi ujanja wanawaibia waziwazi, viongozi wengi mnaowachagua hawana nia njema na nyie.



“CCM  mnayoiona leo si ile ya Mwalimu Nyerere. Heshima ya CCM ilikwisha wakati wa kifo cha hayati Mwalimu Nyerere ambaye alisimamia haki kwa kila mmoja. Viongozi wa CCM waliopo sasa ni walafi tu hawana huruma na wananchi wao” alisema.



Naye mbombea wa udiwani kupitia chama hicho Oscar Ndale alisema pindi atakapopata nafasi kwa wananchi ya kuwawakilisha atahakikisha miradi yoteiliyopo ndani ya Kata ya Ukumbi anaisimamia kwa umakini ili iwaletee manufaa wananchi.



Alisema atapambana na wale wote wanaotumia rasilimali za umma kwa ubinafsi na kurudisha heshima ya Kata ambayo ina kila utajiri.



“Wamegeuza Ukumbi kuwa ni mtaji wao. Naomba kura zenu ili nikapambane nao huko huko kuhakikisha haki yetu tunaipata. Kodi tunalipa lakini hatuoni faida yake kumbe wapo wachache wanaojinufaisha kupitia kodi zetu. Nitawabana ipasavyo ili tuheshimiane” alisema Ndale.



Licha ya kuwa katika uzinduzi huo kulikuwa na mvua, wananchi walikomaa kusimama kwenye mvua hadi mwisho wa mkutano.

No comments:

Post a Comment