GARI ya abiria aina ya Coaster kampuni ya
another G limegonga mtembea kwa miguu muda mfupi uliopita katika maeneo ya Ihemi Wilaya ya Iringa
Mkoa wa Iringa na kupoteza maisha papo hapo.
Gari hilo lenye namba za usajili T 872 BHV lililokuwa likitokea Iringa kuelekea Njombe limemgonga John Mhelela mkazi wa kijiji
cha Ihemi ambapo inaelezwa kuwa marehemu alikuwa akitoka kilabuni na mara baada
ya kuingia barabarani akakutwa na mauti.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo
wameeleza kuwa ajali hiyo imetokana na mwendo kasi wa gari.
Daima Mlyuka ameongea na mtandao huu kuwa
aliona gari iko katika mwendo kasi japo kuwa mbele kulikuwa na mtembea kwa
miguu dereva hakuweza jambo lililosababisha ajali hiyo.
Imeelezwa kuwa marehemu alikuwa anatoka
katika kilabu maarufu kwa jina la “Denyeka” kilichopo kijijini hapo.
“Marehemu alikuwa anatoka kilabu cha Denyeka
lakini alipoingia barabarani tukaona gari linakuja kwa mwendo mkali,
alipojaribu kulikimbia kwa bahati mbaya likamuwahi kabla hajamaliza barabara
likamgonga. Mwendo wa gari ulikuwa wa hatari kweli maana hata sisi tuliokuwa
tukiangalia hata kama isingetokea ajli ule mwendo ni mkali mno” amesema.
Ajali imetokea majira ya saa 12:30 jioni na
hadi muda huu taarifa zinapelekwa mtandaoni askari wa usalama barabarani
hawajafika katika eneo la tukio huku maiti akiwa amenasa chini ya gari.

No comments:
Post a Comment