masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Monday, June 17, 2013

SIRI YA USHINDI WA CCM NG’ANG’ANGE YAFICHUKA

Siku moja baada ya kumalizika uchaguzi katika kata ya Ng’ang’ange, siri ya ushindi wa chama cha mapinduzi imefichuka. Makada wa chama hicho na wananchi wamefichua siri hiyo kuwa mchezo mchafu uliochezwa ndio uliowapa ushindi huo. Wakisimuliana kilabuni katika kilabu cha pombe cha kwa Mitumba kilichopo katika kijiji cha Mdeke katika kata hiyo ya Ng’ang’ange, wananchi walisema walipewa fedha shilingi 5,000 kwa kila mmoja ili wampigie mgombea wa CCM.

Licha ya kupewa pesa hizo usiku wa kuamkia jumapili ya juni 16, wameeleza pia kuwa wakati wakienda kupiga kura, mabalozi na wenyeviti wa vitongoji walikuwa wanawagawia shilingi 2,000 kila mpiga kura. Akisimulia watu kwa magambo, mke wa aliyekuwa diwani wa kata hiyo kabla ya kifo Felechina Msolla amesema watu wa Ng’ang’ange ni wa pombe tu. “kampeni za hapa Ng’ang’ange ni pombe tu wanaridhika” alisema Msolla.

Msolla alisema licha ya watu kuridhika kwa pombe, Chadema kimesababisha hasara kubwa kwa CCM kutokana na kashikashi zake. "Ila tuseme ukweli Chadema wametupeleka mbio, na tungezembea kidogo tu kutumia mbinu ya kugawa pesa ingekula kwetu” alisema.


Uchaguzi wa diwani uliofanyika katika kat hiyo Namgelesi Msuva (CCM) alishinda kwakura 686 dhidi ya Nafred Chahe (CHADEMA) aliyepata kura 217.

No comments:

Post a Comment