HALI tete katika jijini la Arusha muda huu,Polisi wanapiga mabomu
ovyo,watu waliokuwa wamekusanyika katika Uwanja wa Soweto wakisubiri kuaga miili ya watu
waliofariki dunia katika shambulio la kigaidi wametawanywa kwa mabomu.
Mbali na watu kutawanywa kwa mabomu hayo,Mbunge wa Arusha Mjini
Godless Lema amenusurika kufa huku gari lake likiharibiwa
vibaya na mabomu ya Polisi .
Mwandishi wa Blog hii akiwa eneo la tukio ameshuhudia
majeruhi kibao wakikimbizwa katika Hospitali ya Mount Meru jijini Arusha.
Barabara kuu ya kuingia mjini imefungwa, mabomu yanapigwa kila
kona jijini Arusha risasi za moto zinatumika.
Akizungumza na Blog hii katika eneo la tukio mmoja wa wahanga
wa tukio hilo ,
Agnes Mosha anasema kwamba hajui walipo ndugu zake wawili waliokuwa katika
viwanja hivyo kwa ajili ya kuaga miili ya rafiki zao.
"Dada nisaidie nivuke barabara nikimbie Mount
Meru nasikia kuna dada yangu amepigwa
bomu na hali yake ni mbaya sana ,siwezi
kuvuka dada sina nguvu tena jamani"alilalamika Agnes mbele ya Mwandishi wa Blog hii kisha akapoteza fahamu na kuanguka
chini.
Hata hivyo baada ya Agnes kuanguka chini hakuweza kuinuka huku
watu wakikimbia na kumkanyaga,kulingana na hali kuwa mbaya eneo hilo mwandishi wa Blog hii pia alilazimika kukimbia nakutafuta
eneo la kujificha.
Pia kuna tetesi kuwa katika mapambano hayo kati ya raia na askari
polisi, inasemekana askari wawili wameuwawa ingawa taarifa za kuuawa kwa askari
hao hazijathibitishwa. Kwa taarifa zaidi endelea kutufuatilia.
No comments:
Post a Comment