masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Saturday, June 22, 2013

JAMII YAASWA KUSHIRIKI KUKUZA ELIMU




WANAFUNZI wa chuo kikuu cha Tumaini Mkoani Iringa wameshiriki katika kusaidia ukuaji wa elimu vijijini kwa kutumia nguvu zao katika ujenzi wa maktaba inayojengwa katika Wilaya ya Kilolo.

Wanachuo hao wametoa ushirikino wao kwa asasi isiyo ya kiserikiali ya Tuwafikie Tanzania inayojihusisha na uhamasishaji wa elimu vijini.

Akizungumza na mtandao huu, mhamasishaji wa asasi hiyo Bovan Mwakyambiki amesema jamii itambue kuwa kukua kwa elimu kunahitaji watu wanaojitoa.

Amesema ushiriki wa wanafunzi wa chuo Kikuu cha Tumaini uwe ni mfano kwa jamii na kutumia muda wao katika kukuza vipaji hasa katika elimu.

Amese jamii yetu itakuwa na uwezo wa kujitegemea endapo itakuwa  na akili ya kung’amua mambo na upambanuzi wa mambo mbalimbali katika maisha ya kila siku.


Maktaba hiyo inajengwa katika maeneo ya Lugalo Wilaya ya Kilolo ambapo itakuwa ikitoa huduma kwa kila mtu hasa elimu ya jamii kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment