masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Monday, June 17, 2013

CCM Ng’ang’ange wameingia katika mgogoro wa wao kwa wao


Chama cha Mapinduzi (CCM) kata ya Ng’ang’ange wameingia katika mgogoro wa wao kwa wao baada ya kuwahujumu mawakala wao. Hujuma hiyo imetokana na chama hicho kutumia majina ya watu wengine kwa mawakala waliopewa nafasi za uwakala uwakala. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Batista Mnyalape alisema jina lake limehujumiwa japo kuwa tume ya uchaguzi ililipitisha. ”Walitangaza nafasi hizo nikaomba na jina likapitishwa lakini baada ya majina kurudishwa kamati ya siasa ya kata wamelificha na kumpa mtu mwingine. Kweli nimeamini kuwa CCM ni chama cha wababaishaji na wahujumu” alisema. Alisema ingawa yeye ni mwana CCM, ameamini kuwa chama hicho ni chama cha wababaishaji na wahujumu. Kwa mujibu wa majina ya mawakala waliopitishwa na tume ya uchaguzi, jina la Batistani Mnyalape ni la 7 kati ya majina 28. uchaguzi mdogo wa diwani unatarajiwa kufanyika Juni 16 mwaka huu.  

No comments:

Post a Comment