Monday, June 10, 2013
SHERIA ZA NCHI YOYOTE HAZIBAGUI
Sheria za nchi yoyote hazibagui mtu kulingana navyeo au nyadhifa zao. Ikiwa akatokea mtu akaamua kufanya atakalo kinyume na sheria aidha kwa kutumia madaraka aliyo nayo au cheo chake itajulikana kama matumizi mabaya ya nafasi aliyo nayo. Moja ya mfano ninaoweza kuutumia ni askari wa usalama barabarani ambaye jina lake halikujulikana kwa haraka aliyenaswa ana kamera ya mtandao huu maeneo ya Ilula akiendeshwa kwenye pikipiki ambayo haina usajili. Watu wengi wamekuwa wakijiuliza kuwa ni nani hasa ana wajibu wa kusajili chombo chake au kutembelea chombo cha usafiri kilichosajiliwa, swali ambalo huenda likawa na jibu au lisiwe na jibu kulingana na mitazamo tofauti. Swali hilo litabaki chanagamoto kwa wenye mamlaka na wananchi katika kuwajibika katika nafasi zao
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment