masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Friday, June 28, 2013

ASASI YA TUWAFIKIE YAANZA KUJENGA MAKTABA VIJIJINI

Wananchi mbalimbali wakiwa katika shughuli ya ufyatuaji matofali ya ujenzi wa makataba katika kijiji cha Lugalo Kata ya Ilole Wilaya ya Kilolo wakishirikiana na asasi isiyo ya kiserikali ya Tuwafikie Tanzania.



ASASI isiyokuwa ya kiserikali ya Tuwafikie Tanzania inayojihusisha na uhamasishaji wa elimu vijijini imeanza kujenga maktaba katika kijiji cha Lugalo Kata ya Ilole Wilaya ya Kilolo itakayoiwezesha jamii kupata nafasi ya kujifunza mambo mbalimbali ya kijamii.

Ujenzi huo umeanza baada ya taratibu zote za kisheria kufuatwa ambapo ni mwanzo wa ujenzi wa maktaba katika vijijini katika Mkoa wa Iringa.

Akizungumza na mtandao huu katika eneo la ujenzi, mhamasishaji wa elimu vijijini kupitia asasi hiyo Bovan Mwakyambiki alisema mpango huo utakamilika haraka endapo jamii itatoa mchango wa ushiriki.

Amesema jamii inapaswa kujua umuhimu wa elimu na kutumia muda wao kwa kukuza wigo wa elimu kwa watoto na kizazi kijacho.

“Tunaanza ujenzi huu lakini huu ni mwanzo wa uhamasishaji kwa kuwa tunampango wa kujenga maktaba nyingi vijijini huko. Jamii yetu inauhitaji wa kujifunza mambo mengi hasa ya kijamii na hata kilimo kinahitaji elimu.

“Shughuli hii itakwisha haraka endapo jamii itatoa ushirikiano wa dhati ili kufanikisha mpango mzima ikiwa ni pamoj na kutoa michango mbalimbali” amesema Mwakyambiki.

Ametoa wito kwa wale wenye kiu ya kutaka maendeleo kuwa ili kukamilisha ujenzi huo, asasi inahitaji mifuko 300 ya saruji na kwamba ni ruksa kwa mtu yeyote kuchangia.

“Tunaamini wapo wale wenye kiu ya kutaka maendeleo kwa hiyo tunawakaribisha kushiriki nasi ila tunahitaji mifuko ya saruji 300 kama wanaweza kuchangia tunawakaribisha sana” amesema.

Asasi ya Tuwafikie Tanzania ipo kwenye mpango wa kujenga maktaba vijijini katika nchi nzima ili kupanua wigo wa elimu nchini.

No comments:

Post a Comment