MBUNGE wa Iringa mjini Mch. Peter
Msigwa (CHADEMA) ameendelea na msimamo wake wa kuwataka wafanyabishara
ndogondogo Machinga katika maeneo ya Mashine tatu katika Manispaa ya Iringa ili
kupunguza ugumu wa maisha unaowakabili katika familia zao.
Mch. Msigwa ameyazungumza
hayo leo katika mkutano wa serikali uliofanyika stendi Kuu ya Mabasi
uliomalizika hivi punde ili kujadili mwafaka wa wafanyabiashara hao
wanaozuiliwa kwa nguvu ya dola ili wasifanye biashara zao.
Licha ya kuwa mkutano huo ulitakiwa
kuakutanisha viongozi wa Halmashauri na madiwani, Mkurugenzi wa Halmashauri,
Meya pamoja na madiwani wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wamekula kona na kuususia
mkutano licha ya kuwa wananchi walikuwa na hamu kubwa ya kutaka wajibu maswali
yao.
Amesema hajabadilisha msimamo wake
juu ya wafanyabiashara kuendelea kufanya biashara katika maeneo hayo kwa kuwa
maisha yanaendelea kuwa magumu.
“Msimamo wangu haujabadilika wala
haujawah kubadilika. Wafanyabiashara endeleeni kufanya biashara kama polisi
wanataka kuwakamata waje wanikamate mimi tena wanikamatie hapahapa jukwaani
wasije nyumbani kama walivyofanya kwa Lema” amesema.
Akizungumza katika mkutano huo, Mch.
Msigwa alisema kiongozi mzuri ni yule anayefanya jitihada za kutatua matatizo
na si kutumia nguvu kuwaongoza watu.
“Chama cha Mapinduzi wanafikiri
kutatua matatizo ni kutumia polisi kupiga watu tu. Tatizo iliyopo nchini ni
ukosefu wa ajira lakini watu wanapojishughulisha, waache waendelee kupata
chochote kwa ajili ya familia zao na si kuwapiga” amesema Msigwa.
Amesema ni dhambi kuwatumia wananchi
wakati wa uchaguzi na pindi uchaguzi unapokwisha kuwatelekeza bila
kuwasaidia pale wanapotoa kilio chao hususni wapohitaji kuwatumia viongozi
waliowachagua kwa ajili ya kuwapelekea kero zao mbele a maamuzi.
“Wakati wa uchaguzi watu wanatumika
vizuri huku wakiombwa kura kwa kupigiwa kagoti bila kujali mtu an umri gani
lakini uchaguzi unapokwisha wananchi hutelekezwa na hata madiwani huwakimbia
wananchi. Hii ni dhambi kubwa sana” amesema.
Amemtaka kamanda wa Polisi Mkoa wa
Iringa Michael Kamuhanda kutoendeleza tabia yake ya kuleta matatizo ndani ya
Mkoa na kwamba mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha runinga cha
Channel Ten Daud Mwangosi hakijasahaulika.
“Namuagiza Kamuhanda, pamoja na
tuhuma nyingi za kumuua Mwangosi tusingependa atuletee matatizo mengine haka
hayo. Eti kuna usalma gani wa wataifa wanaomshauri Kamuhanda kuendelea kuua
wananchi? Kuwafukuza machinga wasifanye biashara ni kuwauwa wananchi” amesema.
Msigwa amewataka jeshi la Polisi kufanya
kazi kwa weledi bila kushinikizwa na wanasiasa kuwanyanyasa wananchi huku
akisema atachapa fomu za kusaini wale wote ambao haana imani na Kamuhanda ili
apelike hoj binafsi bungeni jmbo lililoibua hisia za watu na kumtaka hata kesho
zipitishwe.
“Nitachapa fomu za kutokuwa na imani
na Kamuhanda ambapo wananchi nitawaomba mzisaini ili nipeleke hoja binafsi”
amesema Msigwa huku wananchi kwa sauti wakijibu “Ndiyooooo!!! Hata kesho”.


No comments:
Post a Comment