masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Monday, May 20, 2013

MCH. MSIGWA APANDISHWA KIZIMBANI NA KUPATA DHAMANA

Mbunge wa Iringa mjini Peter Msigwa (CHADEMA) akielekea kwenye chumba cha mahakama baada ya kushuka kwenye gari. Wanawake wawili mbele yake ni miongoni mwa washtakiwa.

Abuu Changawe maarufu kwa jina la Majeki akiingia mahakamani mara baada ya kushuka kwenye gari.

Mbunge wa Msigwa akiwa amebebwa na wafanyabiashara na wananchi mbalimbali mara baada ya kutoka mahakamani na kuelekea katika ofisi ya chama ya Wilaya.

Mbunge wa Msigwa akiwa amebebwa na wafanyabiashara na wananchi mbalimbali mara baada ya kutoka mahakamani na kuelekea katika ofisi ya chama ya Wilaya.

Mch. Msigwa akiwahutubia wananchi nje ya ofisi ya chama baada ya kutoka mahakamani.
 
MBUNGE wa Iring mjini Mch. Peter Msigwa (CHADEMA) na wafanyabiashara 75 wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya wakikabiliwa na makosa matatu .
Msigwa anakabiliwa na makosa mawili ambapo kosa la kwanza ni la kwake pekee yake na huku kosa la pili likiwahusu washtakiwa wote.
Akisoma mashtka hayo mahakamani hapo leo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya Godfrey Isaya, mwendesha mashta wa serikali Adolf Maganda alisema Peter Msigwa ambaye ni mshtakiwa namba moja anakabiliwa na shtaka la kushawishi watu kutenda uhalifu ambapo alisema Msigwa alifanya ushawishi huo katika mkutano alioufanya Mei 15 Mwaka huu katika maeneo ya mashinetatu.
Kosa la pili ambalo linawakabili watuhumiwa wote 76 limetjwa kuwa watuhumiwa walifanya mkusanyiko pasipo kibali cha polisi na kusababisha uhalifu kufanyika ambapo alisema Mei 19 Mwaka huu watuhumiwa walikusanyika katika maeneo ya mashine tatu bila kibali.
Akisoma kosa la tatu Maganda alisema linawahusu watuhumiwa namba 2 hadi 76 ambapo alisema mnamo Mei 19 Mwaka huu watuhumiwa waliharibu kwa makusudi gari lenye namba za usajili SM 9323 mali ya zimamoto.
Baada ya kusomewa makosa yao, wakili wa kujitegemea ambaye pia ni wakili wa washtakiwa Bazil Mkwata alisema makosa wanayokabiliwa nayo wateja wake yanadhamana na hivyo kuiomba mahakama wataja wake wapewe dhamana.
Akitoa masharti ya dhamana hiyo Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya Godfrey Isaya amewataka washtakiwa kila mmoja kuwa na mdhamini mmoja anayeaminika ambaye anatakiwa kuwa na shilingi milioni moja na kwamba washtakiwa hao wakipewa dhamana wasijihusishe na uhalifu tena.
Hata hivyo mwendesha mashtaka huyo alisema upelelezi haujakamilaka na watuhumiwa 49 wapo nje kwa dhamana baada ya kukidhi masharti ya dhamana huku washtakiwa 27 wakirudishwa rumande baada ya kukosa dhamana na kesi hiyo itatajwa tena Juni 3 Mwaka huu.
Washtakiwa hao wamepandishwa kizimbani siku moja baada ya kukamatwa katika purukushani za askari kuzuia wafanyabiashara ndogondogo (Machinga) kufanya biashara zao katika maneo ya mashinetatu.
Katika mkutano wa kiserikali uliofanyika 19 Mei Mwaka huu katika maeneo ya Mashinetatu Msigwa alisisitiza Machinga kutoondoka katika maeneo hayo ili waweze kufanya biashara kwa ajili ya kupata chochote kwa ajili ya familia zao.
Mara baada ya kutoka mahakamani wafanyabiashara na wananchi walimbeba mbunge wao hadi ofisi ya chama iliyopo Msindo ambako aliongea na wnanchi.
Akiongea na umat wa wananchi Msigwa aliwashukuru wananchi kwa ushirikiano waliouonesha kwake na kwa wafanyabiashara tangu mwanzo wa tukio hadi mwisho kwa kile alichosema wameonesha uzalendo wa dhati.
“Ninawashukuru sana wananchi kwa uzalendo wenu japo kuwa kuna watu wangu wamekosa dhamana lakini nawaahidi kuwa kesho (leo) nitafanya jitihada zozote kwa kushirikiana na viongozi wenzangu kuwatoa. Ila niwatoe wasiwasi kuwa waliobaki watatoka” amesema Msigwa.
Kwa upande wake wafanyabiashara wamemfananisha Msigwa na Mwalimu Nyerere kwa moyo wake wa dhati na upendo wa kweli kwa kile walichosema kuwa akisema ndicho anachofanya.

No comments:

Post a Comment