| Diwani wa kata ya Miyomboni Kitanzia Jescar Msambatavangu aliyekaa akizungumza na wanahabari leo katika ofisi za Klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Iring. |
DIWANI
wa Kata ya Miyomboni – Kitanzini Jescar Msambatavangu (CCM) amesema suala la
wafanyabiashara ndogondogo (Machinga) wanaofanyia biashara zao Mashinetatu
katika Manispaa ya Iringa linazungumzika.
Amesema
hayo leo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ya chama
cha waandishi wa habari Mkoa wa Iringa (IPC).
Amesema
bado kuna haja ya kukaa mezani kwa ajili ya kufanya majadiliano ili kulimaliza
suala la machinga ili waendelee kufanya
biashara zao kwa uhuru.
Amesema
japo kuwa kuna haja ya kukaa mezani bado kuna ugumu wa machinga kuendelea
kufanyia biashara barabarani kutona na ongezeko la matumizi ya barabara na kkwa
ustawi wa jamii.
“Kuna
hali ya ugumu sana
kwa machinga kuendelea kufanyia biashara zao mashinetatu kwa sababu ni barabara
ambayo ongezeko la matumizi limekuwa kubwa” amesema.
Msambatavangu
ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Iringa amesema
kuendelea kuwaacha machinga barabarani siyo vyema kwa usalama wa maisha yao na watu mbalimbali.
Amewataka
wananchi kutoa mtizamo wa kisiasa kuwa mashinetatu kunafanyika kisiasa kwa kuwa
bado kuna uhitaji wa matumizi ya barabara kwa kazi zingine.
“Tunachoangalia
siyo maopato tu bali ni ustawi wa watu na maisha ya watu; nimezunguka maeneo
yote ya Manispaa na kuona Mlandege kuwa kuna uafadhali ndiyo maana tunawaambia
waende kufanyia biashara zao huko” amesema.
Alisema
kutokana na uhaba wa barabara ndani ya Manispaa unaotokana na ongezeko la
matumizi mbalimbali, barabara zinaendelea kujengwa ambapo zinafanyika jitihada
za kukarabati barabara zinazounganisha mitaa ili kufungua upitikaji wa magari
yanayoweza kusababisha msongamano.
No comments:
Post a Comment