masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, May 21, 2013

BARABARA YA IRINGA - DODOMA KUZINDULIWA

Mkuu  wa mkoa  wa Iringa Dkt Christine Ishengoma akizungumza na  wanahabari ofisini kwake leo





RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya  Kikwete anatarajia kuweka  jiwe la msingi katika  ujenzi  wa barabara  ya Iringa -Dodoma  kesho

Akizungumza na  waandishi  wa habari ofisini  kwake   leo Mkuu  wa Mkoa  wa Iringa Dkt Christine Ishengoma amesema  Rais Kikwete  ataweka jiwe la Msingi upande  wa Iringa kesho (Mei 22 Mwaka huu) majira ya saa 3 asubuhi katika  eneo la Migoli  na baada ya hapo mchana ataweka  jiwe la Msingi katika eneo la Fufu Escepment upande wa Dodoma.

Dkt  Ishengoma  amewataka  wananchi  kujitokeza  kwa wingi katika uzinduzi  huo ili waweze kushuhudia uwekwaji wa jiwe hilo.

Pia amesema ujenzi wa barabara hiyo utarahisisha usafiri  wa mikoa  ya  Kusini na Kaskazini mwa Tanzania ambao ulikuwa mgumu na kuwafanya wasafiri kutumia gharama kubwa.

Hata hivyo amesema kuwa ujenzi  wa barabara  hiyo umegawanyika katika maeneo matatu  ambayo kwa upande wa Iringa  imegawanyika  katika sehemu mbili  ikiwemo ya Iringa - Migoli yenye urefu  wa  kilometa 95.2 na Migolo na sehemu ya pili kutoka Fufu Escapement  ikiwa na urefu  wa Kilometa 93.2   wakati  kutoka Fufu Escapement - Dodoma 90 .9 wakati  thamani ya  ujenzi  wa  barabara  hiyo  kwa upande wa Iringa  katika maeneo hayo ni kiasi cha shilingi bilioni 84.2  fedha hizo ni malipo  ya makandarasi na upande wa usimamizi wa Tanroad ni 14 bilioni na  kufikisha jumla ya shilingi 88 bilioni. 

Hata  hivyo amesema  kuwa ujenzi wa barabara  ya Iringa - Dodoma unatarajiwa  kukamilika mwaka 2015 na kufungua  milango ya  kiuchumi katika  Mkoa  wa Iringa na Mikoa ya kusini mwa Tanzania .
  
Akielezea  kuhusu uchakavu  wa  barabara ya Iringa - Dodoma eneo la Mshindo hadi Kihesa Kilolo ambayo pia ni barabara  iliyopo katika mpango  wa ujenzi huo, Ishengoma amesema amemshauri  meneja  wa wakala  wa barabara  Mkoa  wa Iringa kuanza  kuziba mashimo hayo  wakati huu ambao bado ujenzi huo kuanza katika  eneo hilo.

Ujenzi wa barabara ya Iringa - Dodoma utagharimu jumla ya 222 bilioni 

No comments:

Post a Comment