masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Wednesday, May 22, 2013

JK AWEKA JIWE LA MSINGI KATIKA UZINDUZI WA BARABARA YA IRINGA - DODOMA

Waziri wa ujenzi John Pombe Magufuli aliwahutubia wakazi wa Migoli wakati wa uzinduzi wa barabara ya Iringa - Dodoma hii leo.

Rais Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi wa Migoli wakati wa uzinduzi wa barabara ya Iringa - Dodoma hii leo.



RAIS Jakaya Kikwete amezindua ujenzi wa barabara ya Iringa – Dodoma kwa kuweka jiwe la msingi katika kijiji cha Migoli na kuwataka wananchi waendeleze ujenzi huo kwa kuwa waaminifu wa kutunza vifaa vya ujenzi na barabara hiyo kwa ujumla.

Uzinduzi huo ulifanyika leo katika kijiji hicho kilochopo katika Kata ya Migoli Wilaya ya Ieinga vijijini Mkoa wa Iringa ambapo licha ya kuwataka wananchi kuwa waamifu Kikwete amewataka kudumisha amani na upendo kwa kuheshimiana.

“Barabara hii itunzwe, msiibe mafuta na vifuri vya mitambo, tumechelewa sana kuwekeza katika barabara kwa hiyo tukiwa na mitandao ya barabara nyingi nchini tutafungua milango ya uchumi na uchumi utaongezeka” amesema

Amewataka wananchi kutotumia tofauti zao kwa kuliingiza taifa katika machafuko na badala yake amewataka wachape kazi kwa juhudi na maarifa.

“Matukio ya hivi karibuni ni ya kusikitisha sana na hayafurahishi hata kidogo. Watu wabaya tusiwape nafasi kwa sababu watatuingiza katika migogoro mikubwa” amesema.

Wakati huo huo, Waziri wa ujenzi John Magufuli amesema hatakawia kuwatimua wakandalasi watakaozembea na kwenda kinyume na mkataba wa makubaliano.

Amesema hakuna sababu zitakazotolewa juu ya kuchelewa kukamilisha barabara hiyo kwa kuwa tayari wakandalazi hao wamekwisha kulipwa fenda za kufanyia kazi.

“Wakandalasi wameshalipwa fedha kwa ajili ya kujengea barabara hii kwa hiyo hakuna kisingizio. Siwatanii wazembee nitawatimua” amesema Magufuli.

Amesema tangu dunia iumbwe hakuna aliyefikiri barabara ya Iringa – Dodoma kama itajengwa lakini umefika wakati ambao inalazimika kujengwa kwa ajili ya maendeleo ya nchi.

Katika ujenzi wa barabara hiyo ambao utagharimu shilingi 232.2 bilioni, amesema hadi sasa umekamilika kwa asilimia hamsini na tatu (53%) ambapo asilimia arobani na saba (47%) unatarajiwa kukamilika kwa wakati.

Ujenzi wa barabara hiyo umegawanyika katika maeneo matatu  ambayo kwa upande wa Iringa  imegawanyika  katika sehemu mbili  ikiwemo ya Iringa - Migoli yenye urefu  wa  kilometa 95.2 na Migoli, sehemu ya pili ni Migoli – Fufu Escapement  ikiwa na urefu  wa Kilometa 93.2   na sehemu ya tatu kutoka Fufu Escapement - Dodoma 90 .9.

Barabara hiyo inajengwa kwa ushirikiano wa serikali ya Japan, Benki ya Afrika (Africa Development Bank (ADB)) pamoja na serikali ya Tanzania ambapo serikali ya Tanzania inatoa fedha karibu asilimia sitini (60%).

Kwa upande wake Mhandisi Mkuu wa barabara (Tanroad) alisema barabara hiyo inatakiwa kukamilika kwa muda wa miezi 35 ambayo ni takribani miaka 3.

No comments:

Post a Comment