masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Monday, May 13, 2013

MATATU YA SOMALIA YAGOMA


Mkaazi wa Mogadishu atumia baiskeli badala ya basi

 Waendesha mabasi nchini Somalia wamegoma kwa siku ya pili kwa sababu wanasema inabidi wawalipe rushwa wanajeshi wa serikali na polisi katika vituo vya ukaguzi.

Madereva wa mabasi na malori mjini Mogadishu na miji mengine wamekataa kufanya kazi hadi swala hilo limeshughulikiwa.

Kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini Somalia, AMISOM, kimeingilia kati kujaribu kutatua mkwamo huo.

Msemaji wa polisi ameiambia BBC kwamba wanachunguza malalamiko hayo lakini hawana habari kwamba askari polisi wanadai hongo.

Chanzo: bbc swahili

No comments:

Post a Comment