masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Saturday, May 11, 2013

KILOLO WATAKIWA KUWATUMIA WATAALAM WA MISITU KUVUNA MISITU YAO

Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Gerald Guninita



MKUU wa Wilaya ya Kilolo Gerald Guninita amewataka wananchi wa Wilaya hiyo kuwatumia wataalam wa misitu katika uvunaji wa misitu yao ili kulinda mazingira.

Ameyasema haya ofisini kwake katika mahojiano maalum na mtando huu juu ya ushiriki wa kuhifadhi mazingira.

Guninita amesema licha ya kuwa kila mtu ana haki ya kuvuna msitu wake kwa matumizi mbalimbali, kuna haja kubwa ya kuwatumia wataalam wa misitu ili kupata ushauri jinsi ya uvunaji na miti inayopaswa kuvuna.

Amesema japokuwa kila mtu ana msitu wake, si kila mti unatakiwa kuvunwa na kuna kiwango cha ukomavu wa mti unaopaswa kuvunwa.

“Kwanza niwashukuru sana wale wote ambao wamepanda miti kwa sababu hiyo ndiyo kampeni ya utunzaji mazingira tunayoihamasisha ndani ya wilaya yetu. Upandaji wa miti uwe endelevu. Lakini ninawaomba wananchi waelewe kuwa, tunakubali kuwa msitu alioupanda ni mali yake lakini anapotaka kuvuna kwa matumii mbalimbali, awasiliane na wataalam wetu wa misitu ili waweze kumshauri namna ya uvunaji na miti gani inapaswa kuvunwa” amesema Guninita.

Amesema ukiukwaji wa uvunaji wa miti katika maeneo mbalimbali utachukuliwa hatua za kisheria kwa kuwa unachangia maingir kuharibika na kupoteza sura.

“Kuwa na miti ni yambo muhimu kwa kuwa mazingira yetu yanakuwa safi na salama, hewa inakuwa nzuri na ongezeko la joto linapungua lakini miti na misitu kwa ujumla inapokatwa bila utaratibu, hali ya hewa inaharibika” amesema.

Amesema wapo baadhi ya watu ambao wamekwishapata onyo kama fundisho kwa kukiuka utaratibu wa kuvuna miti na kusema endapo atajitokeza mtu anavuna kinyume cha utaratibu atachukuliwa hatua kali a kisheria.

“Tunapenda watu wetu wawee kutumia mali zao kwa ajili ya kuendesha maisha yao lakini mali hizo pia zinatakiwa kutumika kwa autaratibu. Kinyume na hapo hatua za kisheria inafuata japo kuwa ni mali yake” amesema.

Wilaya ya Kilolo imepanda miti aidi ya ekari 10 kwa ajili ya kuendeleza uhifadhi wa mazingira na kwamba mkakati huo unaendelea.

No comments:

Post a Comment