masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Monday, April 22, 2013

MWENYEKITI WA MTAA WA NGOME AZIDI KUANDAMWA



MKAKATI  wa kumng’oa Mwenyekiti wa Mtaa wa Ngome Kata ya Kihesa katika Manispaa ya Iringa Elizabeth Mkayula unazidi kushika kasi baada ya ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa kumwandikia barua mwenyekiti huyo kutaka akabidhi nyaraka za ofisi.

Taarifa zilizoufikia mtandao huu zimeeleza kuwa mkakati huo unalenga kulinga ubadhilifu wa fedha na vifaa vya ujenzi katika soko jipya linaloendelea kujengwa katika mtaa huo.

Akizungumza kwa masikitiko makali, mmoja wa kamati ya ujenzi wa soko hilo aliyeomba jina lake lisiandikwe alisema mkakati huo ni wa makusudi ambapo ni watu wachache waliopanga kaufanya hivyo kutokana na mwenyekiti huyo kuwa muwazi kwa wananchi.

Amesema kutokana na taarifa zilizosomwa kwa wananchi juu ya ujenzi huo, zinatia shaka kwa kuwa mipango yote inajulikana na kuwa taarifa ni za uongo.

“Ni kwamba umetokea wizi mkubwa wakati wa ujenzi wa jengo la vyoo katika soko hilo. Mwenyekiti hakushirikishwa kwa kila kitu ndiyo maana wanafanya kila linalowezekana kumuongoa mwenyekiti ili wachukue mhuri kugonga nyaraka wanazotumia kwa kuiba ionekane mwenyekiti alishiriki. Mimi nikiwa mmoja wa wanakamati ya ujenzi sikubaliani kabisa na sitasaini gharama wanayosema imetumika kujenga kile choo kwa sababu ninajua kila kitu” kimesema chanzo hicho.

Kwa nyakati tofauti wakazi wa mtaa huo wameeleza kuwa utendaji wa kazi wa ofisa mtendaji wa mtaa huo Eliques Ngakonda unatia shaka kwa sababu amekuwa akitumia imla kutaka wananchi wakubali kila taarifa hata kama ni ya uongo.

Wameeleza kuwa ngakonda ameteua baadhi ya watu ambao anashirikiana nao katika kufanya ubadhilifu na kuwatumia hao kumpiga vita mwenyekiti wa mtaa ili asiendelee kuwaumbua kile wanachokifanya.

“Jambo la kushangaza ni pale mtendaji wa mtaa anapowateua watu wakushirikiana nao wakati mwenyekiti tuliomchagua wananchi yupo halafu hawamshirikishi. Ina maana huyu mtendaji ametuona sisi tuliyemchagua huyu mwenyekiti ni wajinga yeye tu mwenye akili? Sasa tunamwambia kuwa sisi siyo wajinga, kama tulivyompigia kura mwenyekiti huyo ndivyo tutakavyomkataa kuwa hatufai. Wasituletee mambo ya ajabu hapa” amesema mwananchi mmoja.

Hata hivyo imeelezwa kuwa chanzo cha mgogoro huo ni ofisa huyo kutompenda mwenyekiti kutokana na msimamo wake kuwa ni wa haki kwa wananchi waliomchagua.

“Mwenyekiti tuliyemchagua sisi hatolewi kama nyanya kwenye matenga ila tukimchoka tutamtoa. Tunawashangaa wanamtoa wao kama nani! Kwanza mtendaji mwenyewe si muadilifu anataka atumie nafasi hiyo kutuburuza! Atatoka mwenyewe badala ya mwenyekiti. Kwanza sisi hatumjui aliyemchagua yeye na tunaweza kumtimua mtaani hapa mara moja kuliko yeye anavyofikiri” kimesema chanzo hicho.

Mtandao huu umefanikiwa kunasa barua iliyoandikwa katika ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa kumtaka mwenyekiti huyo kuwasilisha nyaraka za ofisi.

Katika barua hiyo yeye kumbukumbu namba IMC/A.50/06/37/33 iliyoandikwa Aprili 17, 2013 na kusainiwa na Erasto N. Kiwale kwa niaba ya mkurugenzi anamtaka mwenyekiti huyo kuwasilisha nyaraka zote za ofisi.

Hata hivyo barua hiyo haielezi makosa yaliyosababisha mwenyekiti huyo kuondolewa katika nafasi hiyo.

Alipotafutwa kutolea ufafanuzi juu ya kuondolewa katika nafasi hiyo, mwenyekiti wa mtaa huo Elizabeth Mkayula amethibitisha kupokea barua hiyo na kueleza kuwa kosa lake halijui.

“Kweli nimeamini kuwa ukiwa mkweli kwa wakati huu unageuka kuwa adui wa baadhi ya watu. Ni kweli nimekabidhiwa barua kunitaka niende kukabidhi nyaraka za serikali za mtaa lakini kosa langu silielewi. Lakini ninachoweza kusema ni kwamba, kuandamwa kwangu kulianza baada ya kuuzwa kiwanja cha wazi. Diwani pamoja na mtendaji waliuza kiwanja cha wazi nikaamua kufuatilia, walipoona nimelikalia kidete ndipo wakawatengeneza watu wao waanze kunipiga vita” amesema Mkayula.

Hata hivyo, alipotakiwa kutolea ufafanuzi juu ya ubadhilifu wa vifaa vya ujenzi alithibitisha na kusema ni moja ya sababu inayomfanya sasa hivi kutengenezewa mikakati ya kuondolewa ili lisijulikane kwa watu.

“Kuna makubwa zaidi ya hilo unaloniuliza kwani sikushirikishwa kwa lolote katika ujenzi wasoko. Wanaogopa kunishirikisha watashindwa kuiba kama ambavyo wamezoea kuiba. Ila kuna baadhi ya nyaraka wanazotaka nirudishe mhuri ili wazigonge kwa sababu wanaona kunijia kwa ajili ya kugonga mhuri nyaraka hizo nitawaumbua. Walionichagua ni wananchi ambao wana mamlaka ya kunitoa wakati wowote tena nikisia kuwa wananchi hawanitaki, nawajibika mwenyewe sisubiri kuwajibishwa” amesema Mkayula.

No comments:

Post a Comment