| Mbunge wa Iringa mjini Peter Msigwa akiongea na wakazi wa mtaa wa Lukosi Kata ya Mkwawa Manispaa ya Iringa. |
MWENYEKITI wa Mtaa wa Likosi
Kataya Mkwawa katika Manispaa ya Iringa Kened Mahona (CCM) amekaangwa na
wananchi mbele ya Mbunge wa Iringa mjini Peter Msigwa kutokana na madai kuwa
anatumia kuwaongoza.
Mahona aliingia kikaangoni jan baada
ya wananchi kumsimamisha Mbunge alipokuwa anakwenda msibani baadaya mkutano
uliopangwa kufanyika katika mtaa huo kuahirishwa baada ya msiba kutokea.
Wakimtaka Mbunge Msingwa
kuwasaidia, walisema pamojana mkutano kuahirishwa wanamuomba awasilikilize japo
kwa dakika chache kutokana na mateso na manyanyaso wanayoyapata kwa mwenyekiti
huyo.
Kitoa malalamiko hayo, wananchi
walisema mwenyekiti wao anatumia mabavu katika kazi yake hata kutumia madaraka
yake kuuza ardhi ya wazi na pesa kuweka mfukoni mwake na kila anapotakiwa
kutoleamaelezo anapanga mbinu za kuwabambika kesi wanaoonekana kuwa na nguvu ya
kuhoji.
Wananchi hao wakiwa na jazba
walisema wameamua kutoa malalamiko kwa Mbunge wao ili awasaidie vinginevyo
itafikamahala mwenyekiti huyo atakula kichapo.
“Kuna mambo mengi hapa mtaani
tumekuwa hatutendewihaki lakini mwenyekiti huyu tukimuuliza anakuwa mkali na
kutuambia kuwa tuna fujo na kututishia kukamatwa kuwekwa ndani. Hivi huu
nndioutaratibu wa uongozi? Tunakuomba Mbunge wetu utusaidie” alisema mwananchi
mmojana kupigiwa makofi na wenzake.
Ilielezwa kuwa mwenyekiti huyo
hajawahi kusoma mapato na matumizi na kila akiulizwa anakuwa mkali bila kutoa
majibu huku ofisi akifungua akipenda.
“Imepita miaka mingi mapatona
matumizi hatujawahi kusomewa. Tukitaka kuhoji, mwenyekiti ni mkali kama mbogo. Kama anabisha
aseme hapahapa” alisema mwanachi mwingine.
Kwamba, “tunaeleza kwa masikitiko
makubwa kwa sababu malalamiko yetu hata Mkurugenzi anayafahamu lakini hakuna
utekelezaji. Tunajiuliza kuwa sisi ni miongoni mwa wananchi walipa kodi au sisi ni wakimbizi?
Tunachofanyiwa katika mtaa huu kinatufanya tujihoji mara nyingi bila kupata
majibu. Tunakuomba Mbunge leo utusikilize kilio chetu” alisema.
Mbunge Msigwa alitumia kazi ya
ziada kuwatuliza hasira kwanza wananchi hao kabla ya kumpa nafasi Mwenyekiti
ili ajieleze na kujibu madai ya wananchi.
Alipotakiwa kujibu madai hayo
Mwenyekiti Mahona alisema hawezi kuzungumza chochote kwa kuwa mkutano umeahirishwa
na kutaka utakapofanyika atakuwa na nafasi kubwa ya kutoa ufafanuzi.
Kutokana na mjibu hayo, wananchi
walipandisha hasira na kutaka kutembeza kichpo mbele ya Mbunge jambo
lililomfanya Msigwa kutumia busara kuwatuliza na kuwataka wawe na subira hadi
watakapotangaziwa mkutano.
Wakati huo ofisa mtendaji wa mtaa
huo Neema Kizwi aliyekuwa jirani, alilazimika kusimama mguu pande kuhofia
kibano hicho kisije kikamgeukia.
Hata hivyo wanchi wamelalamika
kuwa eneo la Chuo Kikuu cha Mkwawa limekuwa ni kijiwe cha vibaka ambao
wanawatesa watu kwa kuwapiga nondo na kuwapora mali zao jambo ambalo Msigwa
alisema linazungumzika na kutafutiwa ufumbuzi baada ya kujadili na uongozi wa
chuo hicho.
Awali Mbunge Msigwa alikuwa
afanye mkutano wa kiserikali katika viwanja vya
mtaa huo lakini ukaahirishwa baada ya kutokea msiba jirani na viwnja
hivyo.
No comments:
Post a Comment