masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Thursday, April 11, 2013

MKURUGENZI WA MANISPAA YA IRINGA ATISHIA KUFUKUZA WAFANYAKAZI MASHABIKI WA VYAMA PINZANI

Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa Theresia Mahongo.

MKURUGENZI wa Manispaa ya Iringa Theresia Mahongo amelalamikiwa kufanya kikao na wafanyakazi kuwatisha kuwa wasipokipenda Chama cha Mapinduzi (CCM) watafukuzwa kazi.

Katika kikao chake alichokifanya na wafanyakazi  hao katika ukumbi wa Wellfair  Aprili 4 majira ya mchana, Mahongo alisema kuwa ni marufuku kushabikia vyama vya upinzni na iwapo itabainika kuwa kuna anaeshabikia CCM atafukuzwa kazi. Tanzania Daima limedokezwa.

Imeelezwa kuwa mkutano huo ni utekelezaji wa mikakati iliyowekwa kwa ajili ya kuwabana wale wanaoshabikia vyma vya upinzani kote nchini ikiwa utekelezaji huounaanzia kwa wafanyakazi serikalini.

“Tuliambiwa kuwa kutakuwa na kikao katika ukumbi wa Wellfair ambapo baada ya kufika katika kikao hicho agenda iliyoongelewa ni moja tu kututisha wafanyakazi kuwa atakayechabikia vyama vya upinzani anafukuzwa kazi. Hii siyo demokrasia kabisa hata uhuru haupo sasa kwa sababu watu tunabanwa kiasi cha kutokuwa na uhuru wa maamuzi” kilisema chanzo chetu.

Kwamba hali ya ufanyaji kazi inakuwa ngumu kwa kuwa watu wanafanya kazi kwa hofu hata kuongea na watu inakuwa ngumu hususani wanaojulikana kuwa ni wa upinzani wanapofika ofisini na shida zao imekuwa ni vigumu kuwahudumia ipasavyo kwa wakiogopa kuwa watahisiwa kuwa wanajadili siasa.

“Tunashindwa kujua mpango wao ni nini kutumia vitisho kama hivi. Tunajiuliza, kwani wameshtuka nini kutumia njia ya vitisho wakati huko nyuma haikuwa hivyo? Ama kweli mnyonge ni mnyonge tu” kilisema chanzo chetu.

Chanzo hicho kimeeleza kuwa kwa hatua waliyofikia sasa, lawama za kila aina zitakuwa nyingi kutoka kwa wateja kwa kuwa utendaji wa kazi utakuwa ni wa hofu kuwa ni wa kisiasa.

“Tulipofikia na tunakokwenda ni kugumu kwa sababu hata kuwahudumia watu itakuwa ni vigumu jambp litakalosababisha lawama nyingi kutoka kwa wateja wetu juu ya uwajibikaji wetu kwa sababu tutakuwa tunaogopa kuwa ni akina nani tunawahudumia” kilisema chanzo hicho.

Mkurugenzi huyo alipotafutwa mara kadhaa kwa njia ya simu, simu imekuwa ikiita bila kupokelewa mpaka pale ilipobadilishwa simu nyingine ndipo ilipo alipopoikea simu.

Alipotakiwa kutolea maelezo juu ya hilo alisema hajui lolote kwa kuwa ofisi alimuachia mtu yeye akiwa safarini.

“Mimi sijui lolote kwa sababu nilikuwa safarini na ofisi nilimwachia mtu hata niliporudi hakuniambia chochote” alisema Mahongo.

Hata hivyo alisema sheria na taratibu za serikali zinajulikana kwa hiyo kitakachomfukuza mtu kazi ni taratibu na sheria hizo.

“Lakini hata kama sikuwepo, mtu atafukuzwa tu bila sababu? Taratibu na sheria zinajulikana kwa hiyo si mimi nitakayemfukuza bali ni taratibu tu. Ila nikwambie tu kuwa kwa ujumla sijui lolote” alisema Mkurugenzi Mahongo.

Katika hatua nyungine, mratibu wa baraza la vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA) Iringa Aidan Salehe amesema kitendo cha kutumia vitisho kwa wafanyakazi ni ukiukaji wa katiba na sheria za nchi.

“Tunamshauri Mkurugenzi ajenge barabara za Manispaa zilizoharibika badala ya kuitisha vikao vya kuwatisha wafanyakazi. Ingependeza kama anaitisha vikao vya kujenga barabara na kuboresha maisha ya wanairinga badala ya kutumia madaraka yake kwa vitisho” alisema.

No comments:

Post a Comment