| Mwenyekiti wa baraza la vijana wa chama cha Demokrasia na Maendeleo BAVICHA akitoa tamko la kumukemea Kamuhanda juu ya taarifa zake kwa vyombo vya habari. |
KAMANDA wa Polisi Mkowa wa Iringa
Michael Kamuhanda ametakiwa kuacha mara moja tabia ya kutumia madaraka vibaya
kwa kuwazushia wananchi ikiwa ni pamoja na kutumia madaraka yake kisiasa
tofauti na maadili ya kazi yake.
Haya yamezungumzwa leo na
Mwenyekiti wa baraza la vijana wa Chama cha Demkokrasia na Maendeo (BAVICHA)
Mkoa wa Iringa Joseph Nzala Lyata akikanusha taarifa ya Kamuhanda juu ya
Athanas Mongo (mtuhumiwa wa ujambazi) kuwa ni Kamanda wa BAVICHA.
Amesema BAVICHA Mkoa wa Iringa
waesikitishwa na kitendo cha Kamuhanda kujivika jukumu la kuwapachika raia vyeo
ambavyo haviko kwenye utaratibu wa CHADEMA wala BAVICHA kwa kuwa anafanya hivyo
kwa lengo la kujaribu kukipaka matope Chadema.
“Tunapenda kuufahamisha umma kuwa
zilizotolewa na Kamuhanda, RPC wa Iringa na kunukuliwa na baadhi ya vyombo vya
habari kuwa Athanas Mongo (mtuhumiwa wa ujambazi) ni kamanda wa vijana wa
CHADEMA Mkoa wa Iringa ni uongo na uzushi wenye hila za makusudi za kujaribu
kuharibu taswira ya BAVICHA na CHADEMA kwa umma” amesema.
Amesema Mongo si Kamanda wa
Bavicha Mkoa wa Iringa na wala muongozo wa Mabaraza ya Chama unaosimamia
mabaraza yote likiwemo Bavicha kwa upande mmoja na Katiba ya Chadema kwa upande
mwingine haina wala haitambui cheo ambacho RPC Kamuhanda kamvisha Mongo.
“Tunavyojua sisi hicho ni cheo
kinachotumiaka na chama cha mapinduzi (CCM). Sasa labda RPC Kamuhanda ni mzoefu
wa kukariri vyeo vya CCM. Yeye anajua hilo”
alisema na kwamba “Mongo ni mwanachama wa kawaida wa CHADEMA na BAVICHA na asiyekuwa
na cheo chochote ndani ya BAVICHA wala CHADEMA. Ni mtanzania mwenye haki ya
kuwa mwnachama wa chama chochote cha siasa. Kutuhumiwa kwake kwa masuala ya
uhalifu hakupaswi wala hakuwezi kuhusishwa na Chadema wala Bavicha” amesema.
Amesema Bavicha wanamuonya
Kamuhanda kuacha mara moja tabia ya kukurupuka na kutokuwa makini katika
utendaji kazi kiasi cha Bavicha ili tu kukidhi haja yake ya kuipaka matope
CHADEMA baada ya kushindwa hila hizo kwenye tukio la mauaji ya mwandishi wa
habari, marehemu Daudi Mwangosi kule Nyololo.
“Bila shaka ni ukurupukaji na
kukosa umakini kama huu, ndiyo uliosababisha RPC Kamuhanda akakiuka misingi ya
utawala bora kama ilivyoelezwa na ripoti ya
uchunguzi ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala juu ya mauaji ya Mwangosi” amesema.
Amesema kutokana na mauaji ya
mwandishi wa habari, Kamuhanda anajaribu kufanya kila mbinu kutumia nafasi yake
kukichafua Chadema huku akijua kuwa anakiuka utaratibu na anakwenda kinyume na
utawala bora kwa kujisafisha mauaji yaliyofanyika.
“Uchunguzi wa THUB ambacho ni
chombo cha serikali chenye majukumu ya kikatiba na kisheria kuhusu masuala ya
haki za binadamu ulibaini kuwa RPC Kamuhanda mnamo 02.09.2012 alikiuka sheria
ya vyama vya siasa (Cap 258 RE. 2002) kifungu cha 11 (a) na (b) na sheria ya
Polisi (Sura 322) kwa kuingilia kazi za OCD wa Mufindi na kutoa amri ya kuzyia
shughuli za CHADEMA wakati yeye hakuwa “Officer In-charge” wa polisi wa eneo
husika. Kwa maana hiyo aliyoitoa haikuwa halali kwa kuwa ilitolewa na mtu
ambaye hakuwa na mamlaka kisheria kutoa amri hiyo. Haya ni matumizi mabaya ya
mamlaka, hivyo ni ukiukwaji wa misingi ya utawala bora” amesema.
Amesema kutokana na uchunguzi
huo, unaonesha uendaji mbovu wa Kamuhanda, RPC pamoja na polisi wenzake
walioshiriki katika tukio la Nyololo kumuua mwandishi wa habari.
“Baada ya kufanya mauaji hayo
Kamuhanda na wenzake walianza kufanya propaganda za kuipaka matope CHADEMA ili
kuwanusuru wao, alipaswa kuwa amejiuzulu au amefukuzwa kazi na kushtakiwa
mahakamani kutokana na tukio hilo
la mauaji ya Mwangosi kama ambavyo Chadema imeshauri mara kadhaa, ikiwemo
kuandika barua kwa Rais Jakaya Kikwete” amesema.
Kamuhanda alitoa taarifa kwa
vyombo vya habari kuwa Kamanda wa umoja wa vijana wa chama cha Demokrasia na
Maendeleo (BAVICHA) mkoa wa Iringa Athanas Mongo anashikiliwa na jeshi la
polisi kwa tuhuma za ujambazi.
Kamuhanda alisema kiongozi huyo
wa Bavicha na wenzake wanatuhumiwa kufanya ujambazi uliotokea Machi 15 mwaka
huu kwa kutumia silaha.
No comments:
Post a Comment