| Baadhi ya wananchi waliofika kumsikiliza Mbunge wao Peter Msigwa. |
| Mbunge wa Iringa mjini Mch. Peter Msigwa akihutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Mwagonjo Ipogolo katika Manispaa ya Iringa jana jioni. |
MBUNGE wa Iringa Mjini Peter
Msigwa (CHADEMA) amesema Rais Kikwete ameshindwa kuwahudumia wazee wastaafu na kubaki
akitoa malalamiko na kuaminisha wananchi kuwa yeye ni kiongozi bora.
Mch. Msigwa aliyazungumza jana
katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Mwagongo Ipogolo
katika Manispaa ya Iringa alipokuwa akipokea kero na maoni kutoaka kwa
wananchi.
Alisema serikali ya Kikwete
imebaki kuwa kichekesho kwa kwa mataifa mengine kwa kushindwa kutoa huduma bora
na kugeuza nchi kuwa ya kihuni kutokana na viongozi wenye fikra mfu aliowateua.
“Kipindi cha Mkapa wazee wastaafu
walikumbukwa kwa kiasi fualani, lakini katika utawala wa Kiwete hana habari
kabisa kuwa nchi hii ina wazee na watu wanaolipa kodi ambazo watu wake wenye
fikra fupi aliowateua wanazitafuna kila kukicha” alisema.
Alisema kutokana na ufupi wa
mawazo ya viongozi, haa usalama wa taifa umechoka kwa kuwa hawawezi kufanya
kazi kwa uhuru kwa sababu ya kiongozi wao mwenyewe kuruhuru ujangili na matukio
yasiyo ya lazima kwa maslahi yake mwenyewe.
“Usalama wa taifa umechoka.
Huwezi kusema una usalama wa taifa wakati ndege za kijangili zinatua nchini na
kubeba Twiga na Vifaru huku wakiona na kubaki waking’aa macho tu” alisema.
Alisema serikali ya Mkoloni
iliwaheshimu wamasai na kuwaachia ardhi kwa ajili ya kufuga wanyama kwa ajili
ya kuendesha maisha yao
lakini cha kushangaza serikali ya CCM haiwathamini tena watu kupitia ardhi na
badala yake wanaofaidi ardhi ni wageni.
“Mmasai alifuarahia mapori wakati
wa serikali ya mkoloni. Tangu serikali ya CCM kuingia madarakani mmasai
huyuhuyu amekuwa akinyanyasika maisha yake yote kwa sababu serikali ya CCM
inamfukuza ili ardhi hiyo wampatie muarabu na watu wengine. Ukiona jirani yako
anaonewa ujue hata wewe unaonewa” alisema.
Ameeleza kuwa kwa ujumla serikali
ya chama cha mapinduzi inamatumizi mengi kuliko uwezo wa watanzania ndiyo maana
mikopo ni mingi kuliko kipato.
Katika hatua nyingine Msigwa
alisema matatizo ya wananchi yanatokana na kuwa na viongozi wapuuzi wasiokuwa
na huruma kwa watu wao na kutumia madaraka yao kwa vitisho.
“Kuanzia leo, namtaka Mkurugenzi
wa Manispaa kuacha tabia ya kuwakusanya wafanyakazi wa umma na kuwataka
waendende kumsikiliza mwanachama wa CCM. Huo ni ukiukwaji wa sheria za kazi na
maadili ya utumishi. Mkurugenzi asifikiri hatujui, tunajua vizuri” alisema.
Alisema badala ya Mkurugenzi huyo
kukaa na kupanga mikakati ya kutatua matatizo ya wananchi amekuwa kikwazo kwa
walipakodi kutuma mgambo kuwanyanyasa wananchi na kupiga alama ya X kwenye
nyumba zao.
“Na kuanzia sasa, sipo tayari
kuona mgambo wanawanyanyasa watu barabarani eti wanafanyafanya biashara
kinyume. Kama wanafanya biashara kinyume mbona
ushuru wanapokea? Sipo tayari kuona watu wanabomolewa nyumba zao wakati kodi za
majengo hayo wanazipokea. Wananchi, unganeni pamoja na muhakikishe mtu yeyote
asiwanyanyase. Lakini hata hivyo hakikisheni mfumo wa viongozi tulionao
unabadilishwa vinginevyo tutaendelea kunyanyaswa maisha yetu yote” alisema.
No comments:
Post a Comment