masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Monday, March 18, 2013

WAKULIMA VIONGOZI WAPATIWA MAFUNZO YA KILIMO NA UFUGAJI

Moja ya jengo la chuo cha kilimo kinachojengwa na asasi isiyo ya kiserikali kwa ajili ya kuwakomboa watu wa Kilolo


Miongoni mwa wananchi wa kijiji cha Ukwega Wilaya ya Kilolo Mkoa wa Iringa wanaonufaika na miradi ya asasi isiyo ya kiserikali inayojishughulisha na maendeleo ya watu wa Kilolo (MAWAKI)


WAKULIMA viongozi wametakiwa kuzingatia maelekezo na maagizo ya wataalamu ili waweze kuwa msaada kwa wakulima wenzao kwa ajili ya kuresha kilimo chao.

Hayo yamezungumzwa na Daniel Kalinga Mkurugenzi wa asasi isiyo ya kiserikali inayojishughulisha na maendeleo ya watu wa Kilolo (MAWAKI) wakati wa mafunzo kwa wakulima viongozi yanayofanyika katika ukumbi wa tabasamu Pomerini.

Kalinga ameeleza kuwa MAWAKI imeamua kututoa mafunzo ka viongozi wakulima ili kuongeza uelewa wa wakulima vijijini kwa ajili ya kuboresha kilimo kutokana na kuwa na uhaba wa wataalamu ambao inakuwa ni vigumu kuwafikia wakulima wote.

Kalinga ambaye pia ni mratibu wa mradi mpya wa kutegemeza uhakika wa chakula na maendeleo endelevu amesema yanakwenda sambamba na utoaji elimu kwa wafugaji ili waweze kujikomboa kupitia mifugo bora.

Ikiwa washiriki 30 kutoka vijiji 10 wanapata elimu hiyo kwa muda wa wiki moja, wakufunzi mbalimbali kutoka ndani ya mkoa na nje ya mkoa wamepewa nafasi kwa ajili ya kutoa elimu hiyo.

“Huu ni mwanzo tu wa mafunzo ambapo tunajipanga kutoa mafunzo kwa watu wengi ili kuwawezesha wakulima wengi kufikiwa na elimu kiurahisi bila kutegemea wataalamu pekee. Tumeona tukitumia njia hii inaweza kusaidia kwa kiwango kikubwa kwa kuwa elimu ndogo inayotolewa itawasaidia wengine” amesema Kalinga.

Washiriki hao wametoka katika vijiji 10 vya Kata za Ukumbi, Mtitu, Ukwega na Kata ya Ng’uluwe (Pomerini).

Mbali na utoaji elimu kwa wakulima na wafugaji, asasi hiyo inatoa huduma mbalimbali kwa jamii zikiwemo huduma za afya, mazingira na ujasiriamali.

“Tumefanikiwa kujenga kituo cha watoto yatima na wenye ulemavu, tumejenga bweni la wasichana kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha 5 na 6 Udzungwa, tumejenga bweni la wasichana shule ya sekondari Lukani na Kitowo, katika sekondari ya Mawambala tumejenga vyumba 2 vya madarasa, Pomerini tumejenga mabweni ya asichana na wavulana chuo cha ufundi na shule ya msingi Msengela imejengwa kwa nguvu ya wananchi kwa msaada wa MAWAKI” amesema.

Amesema kwa mwaka huu wanasomesha wanafunzi zaidi ya 82 japo kuwa idadi inaweza kuongezeka wakati wowote kutokana na matokeo ya kidato cha 6 yanayotarajiwa kutoka muda mfupi ujao pamoja na uhitaji wa wanafunzi wanaoendelea na masomo ya kidato cha kwanza.

Pia wananchi mbalimbali wananufaika na mradi wa ufugaji nyuki ambapo MAWAKI inawawezesha vifaa mbalimbali vya ufugaji.

No comments:

Post a Comment