masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, March 19, 2013

SI BUSARA KWA WANATAALUMA KUKIMBIA TAALUMA ZAO NA KUINGIA KWENYE SIASA: DC

Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Evarista Kalalu akimuangalia mgonjwa katika hospitali ya Wilaya ya Mufindi

Mkuu wa Wilaya akiongea na baadhi ya wauguzi na wakunga

Baadhi ya wauguzi wa hospitali ya Wilaya ya Mufundi katika maadhimisho ya siku miaka 60 ya uuguzi na ukunga.

WATAALAMU wa kada mbalimbali wakiwemo wa kutoka sekta ya afya inchini wametakiwa kutokutelekeza taaluma zao na kuingia kwenye siasa na badala yake wawajibike katika nafasi zao kwa ukamilifu, haki na usawa.

Haya yalizungunzwa na Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Evarista Kalalu wakati wa maadhimisho ya miaka 60 ya uuguzi nchini.

Alisema wauguzi hawana budi kutumia muda wao kwa ajili ya kuhudumia jamii katika uzalendo wa dhati kwa kuwa bila wao huduma za afya haziwezi kwenda mbele sawia na mpango wa huduma bora.

“Kazi yenu inahitaji uvumilivu mkubwa kwa watu mnaowahudumia kutokana na mitazamo ya watu mbalimbali juu yenu ila tu msikate tama kwani taaluma yenu ni ya pekee” alisema Kalalu.

Hata hivyo alisema uuguzi ni taaluma ambayo haina ushindani kwa kuwa ni huduma inayohitji ujasiri, kujitoa na usiri mkubwa.

“Tunajua kuwa huduma za afya zina changamamoto nyingi kutokana na mazingira na watu wanaohudumiwa ambazo zinakatisha tamaa na kumfanya muhudumu kuacha kazi au kutowajibila lakini kazi yenu ambayo inabeba uhai wa watu msikate tama” alisema.

Kalalu amesema kazi ya uuguzi inakwenda sambamba na haki na wajibu ambapo amewataka wauguzi kuwajibika na kutenda haki kwa kutoa huduma bora bila kubagua.

“Lakini hata hivyo lugha zetu hazijawa nzuri kwa wagonjwa japo kuwa si wote wenye lugha hizo. Tujaribu kushauriana wenyewe kama watoa huduma na kusaidiana ili tusiwe vikwazo kwa wateja wetu. Ukiwa na hasira huko ulikokuwa, usipende hasira yako ukaimalizie kwenye sehemu yako ya kazi kwa sababu hao hawahusiki na jambo lililokukasirisha” alisema.

Amesema kwamba pamoja na mapungufu yaliyosemwa wauuguzi wasiwe sehemu ya mapungufu ya huduma aidha kwa visingizio mbalimbali.

Hospitali ya Wilaya ya Mufindi iliyopo katika mji mdogo wa Mafinga inakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo za ukosefu wa vyumba maalumu vya kulaza wagonjwa, vitendea kazi na uchafu mawodini na mazingira kwa ujumla.

Naye muuguzi mfawidhi wa hospitali hiyo Stephen Haule akisoma taarifa kwa Mkuu wa Wilaya alisema hospitali hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya uchafu katika mawodi ya wagonjwa na mazingira kwa ujumla kutokana na kukosa watu wa kufanya usafi na kuomba kazi hiyo kupewa kampuni binafsi.

“Katika hospitali yetu tunakabiliwa na chanamoto nyingi; kuna uhaba mkubwa wa vitendea kazi, kuna uhaba wa majengo kwa ajili ya kuwalaza wagonjwa kwa mfano hakuna wodi pekee kwa ajili ya majeruhi akinamama pamoja na upungufu wa rasilimali watu (watoa huduma)” amesema Haule.

Kwamba mfumo wa maji safi na maji taka pamoja na umeme haukidhi haja ya watumiaji kutokana na kuongezeka kwa kiasi kikubwa cha watumiaji tofauti na mwanzo ilipokuwa ikitengenezwa.

Naye Mariam Jackson mkazi wa jijini Dar es Salaam anayepta matibabu katika hospitali hiyo amesema vyoo vya hospitali hiyo haviridhishi kutokana na kukosa maji ya kutosha na hata kuzidiwa na uchafu ikiwa ni pamoja na uhaba wa dawa hali inayosababisha usumbufu kwa wagonjwa.

Kwa upande wake muuguzi msaidizi wa huduma za macho ambaye pia ni msaidizi wa muuguzi Mkuu wa Wilaya Michael Sanga alisema wanakabiliwa na uhaba wa wauguzi ambapo wauguzi waliopo wanalazimika kufanya kazi kupita kiwango ndiyo sababu ya kuwa na majibu ambayo si mazuri kwa wagonjwa.

Hospitali ya Wilaya ya Mufindi ina vitanda 170, wauguzi 214 ambapo kwa siku akina mama wanojifungu ni kati ya 20 hadi 32 na inahudumia watu zaidi ya 300,344.

Baraza la uuguzi na ukunga Tanzania lilianzishwa 19 Machi, 1953 ambalo zaidi ya 60% ya wanataaluma wote katika sekta ya afya ni wauguzi na wakunga.

No comments:

Post a Comment