masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Thursday, March 21, 2013

MAKUHANI WASHAURIWA KUADHIMISHA IBADA KWA NIDHAMU



Mapadre wakimwa kwenye maandamano kuingia kanisani kwenye Misa ya kubariki mafuta nyuma ni Mhashamu askofu Tarsisius Ngalalekumtwa wa Jimbo la Iringa.

MAKUHANI wa Kanisa wametakiwa waaminifu na kuridhika na utii kwa kuwa wapole wenye unyenyekevu na na kutokuruhusu tamaa kuwaingia na kufanya kazi kwa busara katika kuwahudumia wanadamukatika safari ya kuutafuta wokovu.

Haya yamezungumzwa leo na askofu wa Jimbo Katoliki la Iringa Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa alipokuwa akihubiri katika Misa ya kubariki mafuta iliyofanyika leo katika Kanisa Kuu la Kiaskofu Parokia ya Kihesa.

Askofu Ngalalekumtwa ambaye pia ni Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania amesema kuhani anayefanya kazi kwa haki na uaminifu kwa kuwatumikia wanadamu bila ubaguzi kwa kuwatakatifuza anawafanya kuwa safi ili kuwawezesha kuufika utakatifu naye kwa kuwafanya hivyo atakuwa mtu wa Mungu aliyekamilika.

“Tunajijua kuwa sisi ni wadhaifu, tunaathirika na hewa chafu ya ulimwengu, tunaishi katika ulimwengu uliojaa kila aina ya uchafu, ninyi msio na daraja lolote la kipadre tunahitaji maombi yenu. Endeeleni kutulea, kutulinda ili mwovu ibilisi asije akaendelea kutunajisi na kutupotosha. Mtuombee ili tuweze kuwalea ninyi ndugu zetu ili tuwe na upendo usio na unafiki. Tuoombeeni ili kuwafanya ninyi kuwa ni vyombo huru katika utumishi na kumtafuta Mungu kwa bidii” amesema askofu Ngalalekumtwa.

Amesema makuhani ni daraja la kuwawezesha wanadamu kuufikia utakatifu wa Mungu ambapo wanatakiwa kuheshimiwa na kuvikwa mavazi ya pekee yanayolinda heshima na busara yake ili waweze kutenda mema daima.

“Makuhani wanatakiwa kuwa washauri wa kiroho kwa wanadamu wenzao ili wawawezeshe kuyafikia makusudio ya Mungu. Watakapokujikubali na kutenda yale ambayo Mungu anayataka, ndipo watakapokuwa watu wa Mungu. Wanapasika kuukumbatia msalaba, Injili toba hizo ndizo silaha za kupambana na mwovu ibilisi” amesema.

Amesema kuwa Makuhani wakumbuke kuwa kazi yao ni kuendeleza kazi yake Kristo ya kuwaokoa wanadamu na kwamba Yesu Kristo lazima habari zake zitazungumziwa wakati wote ulimwenguni.

“Mwaka huu wa Imani uwe ni mwaka ambao kwenu ni wa kutuombea sisi ili tusilegee katika utumishi wetu ili hamu yetu na kazi zetu kwenu zisirudi nyuma bali tuwe na bidii ya kumtumikia Mungu na kumkumbatia bila kuchoka; tujaliwe kuwa walimu wa Sala kwenu, tuadhimishe liturujia kwa nidhamu, tusiwe waigizaji wa kutenda, kujitoe kwa imani na upendo kwenu” alisema.

No comments:

Post a Comment