masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Friday, March 22, 2013

IDARA YA MAJI YATAKIWA KUTOWABAMBIKIZA WANANCHI BILI

Mkuu wa wa Mkoa wa Iringa Christine Ishengoma akiweka jiwe ya msingi katika chanzo cha maji cha Mawelewele.


Kikundi cha sanaa cha Mkwawa magic site kikifanya maagizo katikauwanja wa mkutano yalipofanyikia maadhimisho ya wiki ya maji kijiji cha Mkoga.

Mkuu wa Mkoa wakiwahutubia wananchi katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya maji kijiji cha Mkoga.




MKUU wa Mkoa wa Iringa Christine Ishengoma amewataka mamlaka ya maji Iringa (IRUASA) wasiwabambikie wananchi bili za maji huku wakitaka kuwa makini na kutoa bili za uhalali kulingana na matumizi ya mtumiaji.

Ishengoma ameyasema hayo katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya maji yaliyofanyika katika kimkoa katika kijiji cha Mkoga katika Manispaa ya Iringa.

Amesema kumekuwa na malalamiko ya mara kwa mara juu ya ankara za maji yakidai kuwa bili zinazotolewa na idara ya maji si sahihi na kuwataka wananchi ambao wanaona bili zao sipo tofauti wasiogope kuwaeleza wahusika ili waweze kulimaliza tatizo hilo badala ya kubaki wakilalamika bila kutoa taarifa.

Kabla ya maadhimisho hayo Ishengoma alikwenda kukagua chanzo cha maji cha Mawelewele pamoja na kuweka jiwe la msingi katika chanzo hicho, akafika kukagua tanki la maji Kitasengwa na baadaye kukagua mradi wa ujenzi wa vyoo katika shule ya msingi Mkoga sambamba na kuwahutubia wananchi kijijini hapo.

Ishengoma amewataka wananchi kutunza vyanzo vya maji na miundombinu sambamba na kutoa ushirikiano na wataalamu wa maji ili maji yatakayozalishwa yawe safi na salama kwa afya ya binadamu.

“Mradi huu si wa serikali bali ni wenu wananchi. Kwa hiyo, ninawaomba muutunze na kuulinda ili maji yaweze kudumu na kutumika kwa watu wote. Msiharibu miuundombinu wana kuchafua na kuharibu vyanzo vya maji” alisema Ishengoma.

Amesema endapo kila mtu atawajibika ipasavyo katika sehemu yake katika suala ya maji, kila mwananchi atapata maji safi na salama kwa gharama nafuu.

Awali injinia wa maji Shaban Jellan ambaye pia ni katibu tawala msaidizi sehemu ya maji akisoma taarifa ya mradi huo alisema wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo za uharibifu wa vyanzo vya maji hali inayosababisha maji kupungua na wakati mwingine kupatikana machafu.

Mradi huo hadi kukamilika jumla ya shilingi 427,462,110 zinatarajiwa kutumika ambapo wananchi wanaotarajiwa kunufaika ni wakazi wa Mawelewele, Kitasengwa na Mkoga ikiwa wananchi wanatakiwa kuchangia shilingi 9,530,302.75 sawa na asilimia 2.5 huku serikali Kuu ikitoa shilingi 371,681,807.25 sawa na asilimia 97.5.

Amesema kufikia Aprili 27, 2013 mradi unatarajiwa kuwa uwe umekamilika ambapo hadi sasa wananchi pekee wamekwisha kuchangia shilingi 7,600,000/= kwa ajili ya ujenzi huo.

Mradi ulianza kutekelezwa Januari 28, 2013 kwa muda wa miezi 5 ambao unatarajia kunufaisha wananchi zaidi ya 2392 kwa umbali wa mita 400 kutoka kwenye makazi ya watu.

No comments:

Post a Comment