HALI ya chakula katika vijiji vya Magulilwa, Nega “B” na
Ndiwili vilivyopo Kata ya Magulilwa katika Wilaya ya Iringa, hali ya chakula
hairidhishi kutoka na kupata hasara katika mazao waliyopanda.
Katika nyakati tofauti imeelezwa kuwa hali ya chakula
inaonekana kuwa tete kutokana na mbegu walizozipanda kuwa kuonekana kuwa
zilikuwa feki.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo Hanifa
Mgata mkazi wa kijiji cha Magulilwa alisema hali ya chakula katika kijiji hicho
inatia wasiwasi kutokana na mazao yao
kutokuchanua inavyostahili na kuendelea kuduma licha ya kupandia na kukuzia
mbolea.
“Tumejitahidi sana
kulima kwa kutumia mbolea pamoja na kutunza mashamba yetu lakini hali
inayoonekana haituridhishi. Mahindi yanadumaa lakini baadaye tumeambiwa kuwa
mbegu tulizozipanda hazikuwa halali” alisema Mgata.
Alisema licha ya kuwa na wataalam wa kilimo ambao walikuwa
wakitoa maelekezo kwa wakulima, matokeo yamekuwa tofauti na matarajio yao licha ya kuwa
wametumia nguvu nyingi na gharama kubwa katika uundaaji mashamba, ulimaji na
utunzaji kwa ujumla.
Kwa upande wake Hadson Mvena alisema wanakabiliwa na
changamoto kubwa ya chakula inayotokana na hali mbaya ya mazao ya chakula.
“Tuna hali mbaya ya chakula pamoja na kuwa tulilima. Changamoto
hii inatokana na kuuziwa mbegu mbaya ambayo haijatusaidia. Hatui la kufanya kwa
sababu kama ni maji yamekwisha kumwagika na
hatuwezi kuyazoa. Kwa upande mwingine unawalaumu sana wataalam wetu wa kilimo kwa kuwa
hawakuwa msaada kwetu hata pale walipoona tunanunua mbegu isiyofaa na kutuacha
huku wakijua kuwa sisi tunawategemea wao kitaalam” alisema Mvena.
Alisema haina maana ya kuwepo wataalam wa kilimo wasio
msaada kwa wakulima ambao kwa makusudi wanapoona tatizo hawatoi ushauri.
Katika hatua nyingine mratibu wa baraza la vijana la Chama
cha Demokrasia na Maendeleo Chadema (BAVICHA) Iringa Aidan Salehe amesema
tatizo la mazao linalojitokeza katika vijiji hivyo ni matokeo ya kuwa na
viongozi wasio na mipango mizuri ya kuwasaidia wananchi.
“Tulitarajia uwepo wa viongozi yaani mbunge na mwenyekiti wa
halmashauri, watakuwa na mipango mizuri kwa watu wao ambao ni wakulima lakini
kumbe ni sawa na tu na watu wangeishi bila kuwepo na viongozi” alisema.
Alisema matatizo hayo yanatokana na serikali ya chama cha
Mapinduzi (CCM) kupuuza kilimo katika nchilicha ya kuwepo na kaulimbiu ya
kilimo kwanza na kwamba mapendekezo yao kwa
mkurugenzi wa halmashauri ya Iringa aunde tume ya uchunguzi kuhusiana na tatizo
hilo.
“BAVICHA tumemshauri Mkurugenzi amfukuze ofisa kilimo wa
halmashauri kwa kushindwa kutoa maelekezo ya kitaalamu kwa wakulima kinyume na
wajibu wake unaomtaka asimamie kilimo muda wote na hata mabwana na mabibi
shamba wa kata nao wafukuzwe ili kuleta dhana ya uwajibikaji” alisema.
Licha ya kuwa Mbunge wa jimbo la Kalenga William Mgimwa
(CCM) kuwa mjumbe wa kamati ya kilimo, maliasili na mazingira amelalamikiwa
kutokuwa makini kwa kutoa mkazo kwa watumishi wa kilimo wanaobeba dhamana ya
uwajibikaji kwa wakulima.
“Kwa kuwa CCM imeshindwa kusisitiza watumishi wote
kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chma chama chao kwa vitendo ambapo mbunge
Mgimwa ndiye msimamizi wa ilani hiyo akatika maeneo yaliyoathirika, tafsiri
yake ni kwamba ameshindwa yeye na CCM yake kwa mujibu wa ilani yao Ibara ya 33 kifungu
kidogo B” alisema.
Mmoja wa wataalam wa kilimo katika Kata ya Magulilwa
alipoulizwa juu ya tatizo hilo
alikiri kulifahamu na kwamba hayo ni matokeo ya kupokea maagizo ya utekelezaji
na kufunga nafasi ya kutoa ushauri wa kitaalam.
Mtaalam huyo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe
gazetini alisema kuwa mbegu hiyo waligundua kuwa siyo nzuri lakini walipojaribu
kutoa ushauri waliambiwa kuwa hayo ni maagizo siyo mjadala.
“Tuliiona ile mbegu habridi namba 614 kuwa ni feki lakini
tulipojaribu kutoa ushauri wa kitaalam kuwa ibadilishe, tuliambiwa kuwa
serikali imeshapanga kwa hiyo kilichobaikia ni utekelezaji tu ndiyo maana
tuliamua kukaa kimya kwa sababu tumepewa maelekezo ya kiutendaji” kilisema
chanzo chetu.
No comments:
Post a Comment