![]() |
| Simon Mangula Diwani wa Kata ya Itandula Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa |
DIWANI wa kata ya
Itandula Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa Simon Mangula (CCM), anadaiwa kutumika kupanga mikakati ya
kumfukuza kazi ofisa kilimo wa kata hiyo kwa madai kuwa ni mwanachama wa Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Chanzo cha kuaminika kutoka katika ofisi ya Wilaya kimeeleza
kuwa mikakati hiyo ni mwendelezo wa adhima ya kufukuza ofisa huyo baada ya
kushindikana katika mkutano wa hadhara uliofanyika 18 Februali Mwaka huu katika
kijiji cha Kimilinzowo ulioongozwa na Mkuu wa Wilaya Evarista Kalalu kwa lengo hilo na wananchi kubaini
mbinu hizo jambo walilolipigia kelele.
Chanzo chetu cha habari kimeeleza kuwa, Mkuu wa Wilaya hiyo baada
ya kushindwa kumfukuza katika mkutano wa hadadhara, mbinu zingine za
kichinichini zimeanza kufanyika ili kufanikisha hilo kwa madai kuwa kama lengo
hilo halitatimia, na kasi ya CHADEMA kuendelea kama inavyoendelea sasa, Chama
Cha Mapinduzi (CCM) kipo hatarini.
“Nchi hii kama kweli ina uhuru,
kwa nini mtu asichague kufanya kile anachoona kizuri kwake? Baada ya kuona
wananchi wamegundua mbinu inayotaka kutumika kumfukuza ofisa kilimo wao na
kuipigia kelele waliamua kuahirisha vinginevyo wangelazimisha siku ile kwenye
mkutano wa hadhara wananchi wangechukua uamuzi ambao siyo mzuri. Lakini
wameamua kutumia mbinu nyingine kukaimisha watu uongozi ili lengo lao liweze
kutimia. Kwa upande wangu sioni haja ya kufanya hivyo ila jambo la msingi ni
kuangalia kazi zinafanyika? Tukifanya kazi kisiasa hatuwezi kufika popote. Huu
ni uonezi” kilisema chanzo hicho na kuhoji.
Chanzo hicho kimeeleza kuwa aliyepewa kazi ya kuhakikisha ofisa
huyo anang’olewa ni diwani wa Kata hiyo Simon Mangula pamoja na ofisa mtendaji
wa kata hiyo Ngano Francis aliyekaimishwa kwa ajili ya kufanikisha mikakati
hiyo.
“Diwani huyo ni wa CCM na ofisa mtendaji aliyekamishwa
ameahidiwa kupewa cheo kamaili cha kuwaofisa mtendaji mara atakapo kamilisha
shughuli hiyo” kilisema chanzo hicho.
Katika hatua nyingine 11 Machi mwaka huu, kilifanyika kikao cha
kamati ya maendeleo ya kata hiyo kujadili maendeleo lakini baada ya kuanza
kikao hicho wakaanza kumkajadili ofisa kilimo huyo jambo lililosababisha
wajumbe wa kamati hiyo kutofautiana.
Kwa mjibu wa habari kutoka katika mmoja wa wajumbe wa kamati
hiyo zinaeleza kuwa mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni diwani aliwataka
wajumbe kupiga kura za kutokuwa na imani na ofisa huyo jambo lililowagawa
wajumbe katika makundi mawili yasiyoelewana kufanya hivyo na kikao kuvunjika.
“Kawaida kikao cha kamati ya maendeleo huwa kinajadili maendeleo
siyo watu lakini cha kushangaza siku hiyo mwenyekiti wa kikao ambaye ni diwani
akaanza kumjadili ofisa kilimo wetu na kibaya zaidi tulichoona siyo haki ni
pale walipotutaka wajumbe kupiga kura za kutokuwa na imani naye wakati yeye
hayupo na hajapewa nafasi ya kuzungumza. Lakini hata angepewa kazi nafasi ya
kujieleza kwa upande wetu hatuoni kosa kwake kwa sababu anafanya kazi kwa
kujituma wala hakuna anayemlalamikia kuwa anamuonea. Huu ni uonezi tena wa
machomacho” kilisema chanzo hicho.
Chanzo hicho kimeeleza kuwa agenda zilizoanza kujadiliwa tofauti
na matarajio ni pale ziliposomwa agenda 3 zinazomhusu ofisa kilimo ikiwemo
agenda ya ofisa huyo kuwa mwanachama wa CHADEMA, ofisa huyo kuwahamasishwa
wananchi wasifanye shughuli za maendeleo na kuhamasisha kutokuwepo na amani.
“Agenda hizo zote zilikuwa batili kwetu kwa sababu ofisa huyo
tunamfahamu hajawahi kufanya upuuzi huo wanaomtwisha lakini kuwa mwanachama wa
chama chochote cha kisiasa ni haki yake kikatiba ila tunachoangalia kazi
zinafanyika ipasavyo? Ingekuwa kazi hafanyi hilo ni jingine lakini kazi zinafanyika na
anatumia hata muda wa ziada kuwahudumia wananchi bila kutaka malipo. Uonezi huu
hatutauvumilia na kama watalazimisha kufanya
hivyo, wajue wazi kuwa wao ni chanzo kikubwa cha uvunjifu wa amani katika
maeneo yetu” kilisema chanzo hicho.
Imeelezwa kuwa kikao kilichoshindikana kufanyika baada ya
wajumbe kutofautiana kwa kutakiwa kupiga kura za kutokuwa na imani na ofisa
huyo, sasa kitafanyika 18 Machi Mwaka huu katani hapo kuendeleza kujadili
agenda zilizowatofautisha wajumbe.
Katika mkutano wa hadhara uliofanyika uliofanyika 18 Februali
Mwaka huu katika kijiji cha Kimilinzowo, Mkuu wa Wilaya alijitoa katika mkakati
wa kumfukuza kazi ofisa huyo baada ya kugundua kuwa tatizo siyo ofisa huyo bali
ni serikali nzima ya kijiji na kata kwa ujumla kwa kukandamiza haki za raia
ikiwa ni pamoja na kuuza ardhi bila kuwashirikisha wananchi, kuwatoza faini
pasipo haki na kuwafanyia ubabe pale wanapohoji mapato na matumizi ya vijiji
vyao.
Mwenyekiti wa CHADEMA katika Kata ya Itandula, Titus Kaduma
alisema kwa sasa mikakati hiyo inafanywa na diwani pamoja na ofisa mtendaji wa
kata kwa nia ya kupata vyeo hapo baadaye wakikamilisha zoezi hilo.
“Llakini sisi wananchi hatulali na hatutakubali kuendelea kuona
uonezi huo ambao kimsingi ni matakwa ya watu wachache na siyo wananchi. Ubabe
kama huu hatuuhitaji katika maisha yetu. Sasa imetosha” alisema.
Naye ofisa kilimo huyo, Ngwalanje Emmanuel alipoongea na gazeti
hili alisema hana mengi isipokuwa anasubiri kikao ikatakachofanyika Machi 18
Mwaka huu.
Akiongea kwa njia ya simu, Diwani wa Kata ya Itandula Simon
Mangula amekiri kuwepo na kikao hicho ambacho japo alishindwa kueleza kuvunjika
kwa kikao hicho.
“Sikatai kuwa tulikua na kikao ila kuvunjika kwa kikao hicho
sihui japo kuwa ni kweli ofisa kilimo huyo kazi zake zina mashaka kwa sababu
anafanya kazi za siasa kunadi CHADEMA wakati yeye mtumishi” alisema diwani
Mangula.
Hata hivyo alisema hakuna taratibu za kumfukuzisha kazi kwa kuwa
yeye hana mamlaka ya kumfukuza kazi mtumishi licha ya kuwa ana maamuzi ya
kumchukulia hatua mtumishi anapokwenda tofauti na taratibu za kazi.
Awali, Februari 4 mwaka huu ofisa kilimo huyo aliitwa na Mkuu wa
Wilaya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama kumhoji kwanini anajihusisha na
masuala ya siasa na kumtaka aandike barua ya kuacha kazi jambo alilolikataa na
kusema ni unyanyasaji kwa kuwa utaratibu wa kazi anauelewa, na anaufuata.

No comments:
Post a Comment