KUTOKANA na kushuka kwa elimu vijiji, asasi siyo ya kiserikali ya
Tuwafikie Tanzania imebuni
mbinu ya kukabiliana na tatizo hilo
ili kukuza kiwango cha elimu vijijini.
Akizungumza na gazeti hili jana,
Mkurugenzi wa asasi hiyo Bovan Mwakiambiki alisema wanatarajia kujenga makta
vijijini zitakazosaidia wanafunzi na watu mbalimbali kujisomea kwa muda wote
watakaoamua kusoma kitabu chochote.
Mwakiambiki alisema asasi yake
ilifikia uamuzi huo kutokana na kuwa kwa kiwango kikubwa watu wa vijijini
kieleimu wamesahaulika na kusababisha kuwa nyumba tofauti na maeneo mengine.
Alisema mpango huo unaanza
kutekelezwa katika Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa kwa kujenga maktaba katika
kijiji cha Lugako Kata ya Ilole Tarafa ya Mazombe ambapo tayari taratibu za
ujenzi zinaanza kwa kuwa wamekwisha kupata eneo.
“Tunaanza na madarasa mawili
ambayo kila darasa litabeba watu 50 ikiwa ni mwanzo tu wa utekelezaji lakini
katika ujenzi huo tunashirkiana na kampuni ya ujenzi ya Costan (Costan Company
Limited) iliyopo jijini Dar es Salaam.
Alisema wamechagua kijiji hicho kujenga
maktaba hiyo kwa kuwa asasi bado ni changa kiasi cha kutoanza vijiji vya ndani
zaidi ili kurahisisha utendaji na utekelezaji uimarishaji hadi pale itakapokuwa
imekomaa kuingia ndani zaidi.
“Katika utafiti tulioufanya
tumeona Iringa ina muamko wa elimu zaidi kuliko sehemu zingine ndiyo maana
tunaanza kujenga maktaba hiyo kwenye Mkoa huu ili Mikoa mingine ijifunze
kupitia Iringa baada ya maktaba kuanza kutumika” alisema.
Alisema hiyo ni moja ya
uhamasishaji wa elimu kwa watu mbalimbali pamoja na wadau mbalimbali ili waweze
kutoa michango yao
katika kuinua kiwango cha elimu nchini.
“Maktaba tunayojenga Iringa ni ya
kwanza katika utekelezaji wetu wa uhamasishaji nchini na baada ya kukamilika
kwake itafuatiwa na ile tutakayojenga Ileje mkoani Mbeya. Leongo letu ni
kukamilisha nchi nzima” alisema.
Asasi ya Tuwafikie Tanzanzania
yenye makao yake makuu jijini Dar es Salaam intarajia kutumia jumla ya shilingi
23,288,000/= milioni katika ujenzi wa maktaba hiyo huku bodi ya Huduma za
Maktaba Tanzania
wakiahidi kuchangia viatabu vya ziada.


No comments:
Post a Comment