masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, February 12, 2013

MTU APOTEA NA KUPATIKANA KWA IMANI ZA KISHIRIKINA > Mzee mmoja akamatwa kwa tuhuma za kuhusika > Wananchi wataka aadhibiwe ili uwe mfano kwa wengine


MTU aliyepotea katika kijiji cha Madege kata ya Idete Wilaya ya Kilolo kwa imani zinazosadikika kuwa ni za kishirikina amepatikana katika mazingira ya kutatanisha akiwa na hali mbaya.

Kutokana na tukio hilo, mtu mmoja anayejulikana kwa jina la Limitel Mbombwe amekamatwa na wanachi akituhumiwa kwa kuhusina na kupotea kwa mtu huyo.

Akizungumza katika mkutano wa dharula katika kijiji hicho, Mwenyekiti wa kijiji hicho Philimino Msuva alisema Amuru Kiwone mkazi wa kijiji hicho aliripotiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha Februari 3 Mwaka huu akiwa nyumbani kwake jambo lililosababisha kuitisha msako wa kila mahali.

Alisema wakati wanakijiji wakiendelea na msako, zilianza fununu za mpotevu kuonekana katika nyumba ya Mzee Mbombwe ambaye ni jirani yake hali iliyowafanya wananchi kutoa msimamo kuwa siku inayofuata wataanza kuingia nyumba hadi nyumba kumtafuta mtu huyo.

Kufika Februari 6 Mwaka huu, mpotevu alikutwa asubuhi akiwa hajiwezi huku aliwa hana nguo nje kidogo na yumba ya mtuhumiwa wa tukio hilo bila kuongea chochote ndipo alipochukuliwa na kupelekwa katika huduma za afya na kutoa taarifa kwa wananchi kuwa zoezi la utafutaji lisimame kutokana na kupatikana kwa aliyekuwa akitafutwa.

Akizungumzia juu ya upatikanaji wake kaka yake Amuru (aliyepote) Osward Kiwone alisema anapoamka asubuhi kuangalia upande wa juu jirani na mtuhumiwa alimuona mdogo wake akiwa amelala huku akiwa mtupu.

Wakati wa mkutano huo ambao watu walifurika kusikiliza namna ilivyotokea, mke wa mtuhumiwa Bi Lena Kihongosi alithibitisha kuonekana kwa kiwone aliyekuwa akitafutwa katika sehemu anayoishi mumewe.

“Naomba ulinzi kwenu watu wote mliofika hapa kwa ajili ya tukio hili. Mwenzenu mumewangu sikai naye nyumba moja japo kuwa kuna nyumba mbili sehemu moja. Amejitenga nami lakini wakati watu wakiwa wameacha shughuli zao kwa ajili ya kumtafuta jirani yangu, wajukuu wangu walikuja walikia kutoka sehemu ambayo mume angu anaishi. Nilipowauliza wanalilia nini, waliniambia kuwa wamemuona mtu tunayemtafuta na walipotaka kumuuliza babu yao akawapiga kuwa wasimwambie mtu yeyote” alisema.

Wakati hayo yakizungumzwa binti yake aliyejitambulisha kwa jina la Sikunena Mbombwe alithibitisha tukio hilo kuwa ni la kweli kutokana na vitendo anavyotendewa na baba yake huku watoto wake wakiwa mashahidi.

“Hilo suala ni la kweli. Watoto wangu wawili waliniambia kuwa wamemuona anakoishi Baba yangu. Lakini kutokana na vitendo anavyotendewa mama yangu na ninavyotendewa mimi na Baba huyu vinadhihirisha wazi kuwa ni vya kishirikina. Huu mzee wetu amekuwa kama simba kwani mara kadhaa akitutendea kitu kibaya anatutishia kuwa tutakufa. Siwezi kusema yote kwa sababu hapa kuna watoto na watu wazima pia ila ukweli ndio huo” alisema.

Katika hali ya kushangaza, mtoto wa miaka minne ambaye ni mjukuu wa mzee huyo Wini Kisumbi bila kuogopa watu alieleza kuwa alimuona mtu aliyepotea nyumbani kwa babu yake akiota mto.

“Nilimuona Amuru kwa babu anaota moto wakati watu wakiwa wanamtafuta. Nilipomuuliza babu kuwa mbona nimesikia kuwa wale watu pale ng’ambo wanamtafuta huyu babu akanipiga akasema tusimuite Amuru ila tumuite “Mang’inya”. Nilikuwa na mwenzangu akasema tunakenda kumwambia mama halafu akatupiga kuwa tusiseme. Ila ni kweli alikuwa mwenyewe tunamfahamu vizuri kwa sababu ni jirani yetu” alisema mtoto huyo.

Alipopewa nafasi ya kujitetea Mbombwe alishindwa kukataa na kutiwa hatiani jambo lililowafanya wananchi kumkamata mbele ya uangalizi wa serikali na kufikishwa maktika ofisi ya kata hiyo kwa mahojiano zaidi.

Naye mwenyekiti wa kijiji hicho Philimino Msuva akiongea katika mkutano huo alisema matukio kama hayo hayana budi kukomeshwa kwa sababu yanarudisha maendelea ya watu nyuma.

Tukio la kupotea kwa mtu katika kijiji hicho si la kwanza kwani aliwahi kupotea mwanafunzi wa shule ya msingi na mifupa pamoja na fuvu lake kupatikana katika shamba la miwa la mtu mmoja wa kijiji hicho.

No comments:

Post a Comment