masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, February 5, 2013

"Sijawahi kuwaona ndugu zangu tangu nizaliwe"

Kibaso Msimbiti mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Lyasa anayewatafuta ndugu zake ili afahamiane naye.

Kibaso Msimbiti mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Lyasa iliyopo Kata ya Ifunda Wilaya Iringa hajawahi kumuona baba yake mzazi wala ndugu zake wa upande wa baba yake tangu kuzaliwa kwake kutokana na kufiwa na Mama yake mzazi akiwa bado mdogo.

Akiongea na gazeti hili shuleni hapo, Msimbiti ambaye kwa kabila ni Mkurya alisema anamtafuta baba yake mzazi ambaye hata hivyo jina lake halifahamu.

Alisema kuwa amelazimika kuongea na gazeti hili ili kwa ndugu yeyote atakayekuwa anamfahamu aweze kumtafuta ili wafahamiane hata yule atakayekuwa anamfahamu baba yake mzazi aweze kumsaidia ili kujua alipo.

“Kwa tetesi ninazozipata kutoka kwa ndugu wa marehemu mama nimeambiwa kuwa baba yangu ni fundi magari (mechanic) ambaye ni mwenyeji wa kijiji cha Komge – Musoma” alisema Msimbiti.

Amemtaja marehemu mama yake kuwa alikuwa anaitwa Pelagia Mhelela ambaye alifariki yeye akiwa bado mdogo.

Hata hivyo amemtaja ndugu wa baba yake mzazi kwa jina la Mama Jose Msimbiti ambaye ni mkazi wa Tabata jijini Dar es Salaam.

“Baada ya mama yangu kufariki nilichukuliwa na mapadre wa Kanisa Katoliki hapa Lyasa ambao hadi leo wananilea na kunisomesha lakini natamani sana kuwafahamu ndugu zangu kwa upande wa baba kwani hadi leo simfahamu hata mmoja” alisema.

Msimbiti ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 18 anawaomba wasamaria wema wanaomfahamu baba yake na ndugu zake ili aweze kuonana naye huku akitoa mawasiliano yake kuwa ni 0766-070925 na namba ya mlezi wake Padre Richard Chatila 0787-498942

No comments:

Post a Comment