masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, February 26, 2013

Shule ya Msingi Kitwiru na changamoto zake

Moja ya jengo la Shule ya Msingi Kitwiru lililobomoka. Majengo hayo  yalijengwa tangu mwaka 1953 ilipokuwa ikianza shule hiyo.

Sehemu ya jengo la Shule ya Msingi Kitwiru iliyobomoka.

Sehemu ya jengo la Shule ya Msingi Kitwiru iliyobaki baada ya kubomoka . Sehemu iliyobaki haitumiki kwa hofu ya kuwa inaweza ikaanguka wakati wowote wanafunzi wakiwa darasani na kusababisha ajali kubwa.


Shule ya Msingi Kitwiru iliyopo Kata ya Kitwiru katika Manispaa ya Iringa iko hatarini kukwama kielimu kutokana na kukabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa vymba vya madarasa 6.

Akiongea na mtandao huu leo, mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo Chelestino Mage amesema upungufu wa vyumba vya madarasa hayo unatokana na kuanguka kutokana na uchakavu kwa kuwa majengo yaliyopo ni ya muda mrefu.

Pamoja na upungufu wa vyumba vya madarasa Mage amesema shule hiyo pia ina kabiliwa na upungufu wa madawati 103 pamoja na nyumba 5 za kuishi walimu.

Shule hiyo ambayo ni kongwe kuliko shule zote za Manispaa yenye jumla ya wanafunzi 683, wanafunzi wanakabiliana na changamoto ya ukaaji wakati wa vipindi madarasani kutokana na madawati yaliyopo kutokukidhi haja.

Kwa mujibu wa taarifa zilizoufikia mtandao huu awali zilieleza kuwa shule hiyo ina nyumba za waalimu 6 na kuwa waalimu waliopo wana nyumba za kuishi.

Katika utafiti uliofanywa na mtandao huu, umebaini kuwa kati ya nyumba 6 zilizoelezwa awali, ni mwalimu mmoja tu ambaye anaishi kwenye nyumba ya shule ambamo ameamua kutenga chumba kimoja kwa ajili ya ofisi kutokana na majengo kutojitosheleza huku waalimu wengine wakikosa mahali pa kuishi na kulazimika kupanga mitaani kwa gharama zao.

Mage amesema tayari taarifa hizo zipo katika ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ili kuzifanyia kazi ikiwa ni pamoja na kumpeleka injinia wa Manispaa kwa ajili ya kufanya tathimini ili waweze kuomba michango kwa wazazi na wadau mbalimbali wa maeneo hayo kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Taarifa hizo zilithibitishwa na ofisa mtendaji wa kijiji cha Kitwiru Edgar Mtono kuwa shule ilipo sasa ina hali mbaya kutokana na majengo kuanguka yenyewe kutokana na uzee pamoja na upungufu wa madawati.

“Kiujumla shule ina changamoto nyingi ambazo siwezi kuziorodhesha zote lakini kikubwa ni majengo ya vyumba vya madarasa, madawati na nyumba za walimu” amesema Mtono.

Shule ya Msingi Kitwiru ilianzishwa mwaka 1953 kabla ya kuundwa kwa chama cha TANU. 

No comments:

Post a Comment