masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Wednesday, January 16, 2013

William Lukuvi na Mgimwa lawamani

Mratibu wa Baraza la vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendelo (BAVICHA) Aidan Salehe akiongea na vyombo vya habari katika ukumbi wa Embalasasa Motel.


Waziri wa fedha na uchumi William Mgimwa pamoja na Waziri William Lukuvi wamelalamikiwa kuwatesa wananchi katika majimbo yao kutokana na utaratibu wao mbovu wa kuwatelekeza bila kukumbuka kukutana nao ili kusikiliza matatizo yao.

Haya yamezungumzwa leo na Aidan Salehe mratibu wa baraza la vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA) alipokuwa akiongea na vyombo vya habari juu ya mahangaiko ya wananchi wa majimbo ya Kalenga na Isimani kutokana na upatikanaji wa pembejeo za kilimo.

Salehe amesema mfumo mbovu wa chama cha mapinduzi (CCM) ndio unaowafanya viongozi hao kuwatelekeza wananchi wao bila kujali matatizo wanayokumbana nayo.

Samesema kutokana na mfumo huo, mawakala wa pembejeo ndio wanaoonekana kama ndio wenye dhamana ya kusambaza pembejeo na kugeuza biashara zao hali inayowatesa wananchi katika kufanikisha kaulimbiu ya “Kilimo kwanza”.

“Mfumo mbovu wa serikali ya CCM wa kuwaachia mawakala kusambaza mbolea umeleta matatizo katika Wilaya ya Iringa (V). Hii inatokana na mawakala kuuza mbolea kwa bei ghali sana tofauti na utaratibu wa serikali kutoa mbolea ya ruzuku kama kama wanavyojinadi neon lao “kilimo kwanza” amesema Salehe.

Kutokana na lawama za mratibu huyo, imebainika kuwa pembejeo hizo katika Wilaya hiyo mbolea ya DAP inauzwa shilingi 80,000, Minjingu shilingi 40,000, Urea 70,000 na Mbegu kilo 10 inauzwa shilinigi 45,000 na kutofautiana na bei za mjini ambapo DAP inauzwa shilingi 75,000, Minjingu 20,000, Urea 65,000 na Mbegu kilo 10 ni shilingi 40,000.

Salehe amesema CCM wanakiuka ilani yao ya uchaguzi ya mwaka 2010, ibara ya 31 kifungu kidogo a, b, c, na d.

Katika ilani hiyo inaeleza kuwa CCM wataanzisha Benki ya kilimo ili kutoa mikopo kwa wakulima kukipatia kilimo fedha za kutosha kwa kuhakikisha kwamba bajeti ya serikali haiwi kuzuizi cha maendeleo ya kilimo nchini pamoja kuongeza upatikananji na utumiaji wa pembejeo za kilimo hususani mbolea, mbegu na miche bora na kuweka mfumo utakaohakikisha upatikanaji wa pembejeo hizo kwa wakulima.

Salehe amesema wasimamizi wa ilani hiyo katika majimbo ya Kalenga na Isimani, wameshindwa kusimamia kilimo na badala yake wamegeuka kuwa mateso na mzigo kwa wananchi waliowachagua.

“Kutokana na wabunge hawa kushindwa kusimamia ilani ya uchaguzi, Katiba ya nchi, Katiba yao ya CCM ambayo wanatakiwa wasimamie na kwa kuwa wakulima ndio wahanga kwani waliwachagua kupitia ilani yao” amesema

Hata hivyo amesema mapendekezo ya BAVICHA wanataka serikali iwatangazie wananchi kuvunja kaulimbiu ya kilimo kwanza kwa kuwa haina tija kwa wakulima.

“Tunapendekeza kuwa, serikali iwatangazie wananchi kuvunja kwa kauli mbiu ya “kilimo kwanza” kwani haina msaada kwa wananchi wakulima walio wengi vijijini, wananchi wawatathimini wabunge wao na kuitathmini ilani ya CCM na wajiridhishe kuwa walidanganywa ili ifikapo kipindi cha uchaguzi wasiwapigie kura kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu pamoja na maofisa kilimo wa Mkoa, wilaya pamoja na mabwana shamba wote wawajibishwe kwa kushindwa kuchukua hatua za kurahisisha upatkanaji wa pembejeo kwa wakati” amesema.

Amesema hakuna haja ya CCM kujinasibu kuwa inatekeleza kilimo kwanza wakati wakulima wanakosa pembejeo.

Aidha amemkumbusha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda kuhakikisha anatekeleza kwa vitendo utoto wake wa mkulima  kwa vitendo badala ya kuzungumza kwa maneno.

“Bavicha tunamtaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutekeleza kwa vitendo kifungu cha 52 cha Katiba ya nchi yetu juu ya utekelezaji wa shughuli zake za kila siku kwani ameshindwa kusimamia kilimo nchini mwetu ambacho kimegeuka mradi wa wachache” amesema

Hata hivyo ameitaka serikali kupeleka chakula mara moja katika vijiji vya Kipera, Kiwele, Mgera  katika jimbo la Kalenga pamoja na vijiji vya jimbo la Isimani karibu vyote pamoja na kuitaka CCM kuiga ilani ya CHADEMA ya 2010 – 2015 katika kifungu 4.1.1 ambayo inasema “CHADEMA inaamini katika kilimo bora cha kisasa, na kuwa kilimo kwa sasa na muda mrefu ujao ndio nguzo kuu ya uchumi kwa Tanzania. CHADEMA inaamini pia kwamba ili kilimo kiweze kukua kinavyostahili na
Serikali ya CHADEMA itaangalia uwezekano wa kuanzisha kilimo cha mijini (urban farming) hasa katika mawazo ya bustani za mboga na matunda”.

No comments:

Post a Comment