masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, January 15, 2013

Katibu wa CCM ataka kumpiga mwandishi

MWANDISHI wa habari wa gazeti la Mtanzania Oliva Motto amenusurika kupigwa mahakamani na katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mufindi Jacob Nkomola aliyefikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazo mkabili.

Tukio hilo limetokea leo katika Mahakama ya Mwanzo ya Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, kwa kumvamia Mwandishi wa habari kwa kile alichokiita ni hasira ya kesi yake.

Kizaa zaa hicho kiliianza mara mwandishi huyo alipokuwa akipiga picha mahakamani hapo ikiwa ni sehemu yake ya uwajibikaji katika kazi yake.

Nkomola alifikishwa mahakamani hapo kujibu shtaka linalomkabili la kutishia kuua kwa maneno, kinyume na sheria kifungu namba 89 kifungu kidogo “A”.

Akimsomea shitaka mahakamani hapo Hakimu Zakaria Mushi alisema mshitakiwa alitenda kosa hilo Oktoba 3 mwaka jana (2012) katika eneo la Mkombwe, ambapo alimtishia Alexandel Tweve  mkazi wa Mafinga.

Mtuhumiwa alikana shtaka hilo kisha hakimu akutoa masharti ya dhamana ya ahadi ambayo inathamani ya shilingi laki mbili (200,000/=), na adhaminiwe na mtu mmoja atakayetambulishwa kwa barua kutoka katika ofisi ya serikali ya kijiji au Kata.

Kupitia masharti hayo mshatakiwa alikuwa na mdhamini ambaye hakukidhi vigezo vya kuwa na barua ya uthibitisho kutoka katika ofisi za serikali ya kijiji na hivyo kuzuiliwa kwa muda wa saa moja akiwa chini ya ulinzi.

Kesi imeahirishwa hadi 30 Januari mwaka huu itakapotajwa tena na hakimu alimtaka mstaki  wa kesi hiyo kufika na mashahidi wake aliowaorodhesha

Katika hatua nyingine mara baada ya kesi kuahirishwa  na baada ya mwandishi wa gazeti hilo kutoka nje kwa ajili ya kupiga picha, mtuhumiwa alimfuata mwandishi na kumkuda akihoji ridhaa ya mwandishi huyo kupiga picha.

“Kwa nini unanipiga picha? Nani amekuruhusu unipige picha, kwanza wewe ni nani? Umepokea rushwa huko uje uniandike mimi, na nitaona kama habari hiyo itatoka,” Alihoji Katibu huyo.

Akijibu maswali ya mtuhumiwa huyo mwandishi alisema “Mimi ni mwandishi wa habari, ninafanya kazi kwa maadili, sijakurupuka ndiyo maana nawajibika. Hii ni kazi yangu huwezi kunifundisha wewe leo hapa mahakamani” alisema mwandishi huyo

Hatua hiyo iliwashangaza watu waliohudhuria kesi hiyo katika viunga vya mahakama wakihoji mamlaka ya mtuhumiwa kumfuata umbali wa hatua zaidi ya saba mwandishi, huku mtuhumiwa akiwa chini ya ulinzi kwa kuwa bado alikuwa anashikiriwa kutokana tuhuma pamoja na kutokidhi vigezo vya dhamana yake.

Mwandishi huyo alikimbilia kwa hakimu wa mahakama hiyo akitaka msaada juu ya tujkio hilo, na ndipo hakimu Mushi alimtaka mwandishi huyo kufika kituo cha polisi kutoa taarifa ya tukio hilo.

Akiwa njiani Mwandishi alimpigia simu Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mufindi Cosmas Kaguo ambaye alimuomba mwandishi kuonana naye kabla ya kufika katika kituo cha Polisi cha Mafinga.

Hatua ya mwenyekiti wa CCM Kaguo kukutana na mwandishi huyo kabla ililenga kufanya kikao cha dharura jamba ambalo alifanikiwa kuitisha kikao hicho na kamati ya siasa na kuomba radhi juu ya tukio lililotokea, na baada ya muda wa dakika 20 Katibu wa CCM (Mtuhumiwa) aliingia katika moja ya ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, iliyopo katika ukumbi wa mikutano na kuomba radhi juu ya kile alichokifanya katika viunga vya mahakama.

Ombi la mwenyekiti wa CCM Wilaya, lilikubaliwa na mwandishi huyo kwa kusitisha hatua yake ya kufungua kesi katika kituo cha polisi Mafinga.

Akitoa utetezi wake, mtuhuimiwa huyo alisema “Ninaomba unisamehe sana Oliver, unajua kesi yangu hii niya kisiasa, na kukufanyia hivyo ni hasira baada ya mtu anayenituhumu kutumia njia mbalimbali za kuniangamiza, ninajua nimekukwaza wewe, lakini pia nimeidhalilisha taaluma yako, ninakuomba unisamehe,” Alisema Nkomola.

Hata hivyo baadhi ya wanasiasa Wilayani humo walisema katibu huyo amekuwa akitumia vibaya wadhfa alionao, na kujisahau kama kuna mikono ya sheria, na kuwa nguvu ya kufanya vurugu katika chombo hicho cha mahakama ambacho ni muhimili mkuu wa serikali, ni kutokana na jingo la Mahakama hiyo kuwa ni mali ya chama cha mapinduzi.

“Angekuwa mtu mwingine aliyefanya vurugu Mahakamani angechukuliwa hatua pale pale, kufanya fujo mbele ya mahakama, tena mahakimu wanaona, si jambo la mdhaha, ni kuidharau Mahakama, laki amefanya vile kwanza akijua yeye ni kiongozi mkubwa wa chama Wilayani humo, lakini pili, ni juu ya jingo lao, anaona kama anayo haki ya kufanya chochote yeye kama baba mwenye nyumba wa Mahakama hiyo, lakini si sifa ya kiongozi bora hata kidogo, na kusema nitaona kama habari hiyo itatoka inamaa yeye ndiyo anayezuia na kuruhusu habari?, anataka kutwambia yeye ndiyo mratibu au mhariri wa vyombo vyote vya habari!”  Walihoji.

Kikao cha usuruhishi dhidi ya tukio hilo, kilichukua zaidia ya saa nzima hadi kumalizika kwake, mwandishi huyo yupo wilayani humo kwa siku ya tatu sasa, akifuatilia masuala ya elimu kwa wanafunzi wanaoanza elimu ya kidato cha kwanza, pamoja na changamoto zinazoikabiri sekta ya elimu na Kilimo Wilayani humo.

No comments:

Post a Comment