masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Thursday, January 17, 2013

Mtuhumiwa wa mauaji ya Mwangosi mgonjwa


KWA mara ya tatu mtuhumiwa wa mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha runinga cha Channel Ten Daud Mwangosi hakufikishwa mahakamani kutokana na sababu iliyoelezwa kuwa ni mgonjwa.



Mwendesha mashtaka wa serikali Adolf Maganda ameiambia mahakama leo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Dyness Lyimo kuwa mtuhumiwa asingeweza kufikishwa mahakamani kutokana na taarifa ugonjwa japo kuwa haikuelezwa yupo katika hospitali gani.



“Shauri hili inaletwa kwa ajili ya kutajwa lakini kwa taarifa zilizotufikia ni kwamba mtuhumiwa anaumwa kwa hiyo hatoweza kufika lakini hata hivyo upelelezi bado unaendelea” amesema Maganda.



Hata hivyo kesi imeahilishwa hadi 31 Januari mwaka huu itakapotajwa tena.

 

Siku ya kwanza mtuhumiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo kwa gari la kifahari lenye namba za kiraia T 320 ARC linalosadikiwa kuwa ni la RCO huku kwa mara ya pili akifikishwa kwa miguu na kuondolewa mahakamani hapo kwa gari namba DFP 2175 pick up akiwa katika ulinzi mkali huku waandishi wa habari wakidhibitiwa na polisi na mmoja wao kunusurika kupigwa jambo lililoamsha hisia tofauti miongoni mwa wananchi wengi mkoani hapa.



06 Desemba mwaka jana mtuhumiwa huyo hakufikishwa mahakamani kutokana na sababu iliyotolewa kuwa gari la kusafirishia mahabusu limekosa mafuta.



Katika hali isiyo ya kawaida, mtuhumiwa huyo mwenye namba G 2573 akiwa mahakamani hapo alipandisha hasira na kutaka kumpiga mwandishi wa gazeti hili aliyekuwa akipiga picha mahakamani hapo.



Pasificus akiwa na jazba alisikika akisema “watu tuna uchungu na kesi halafu wewe unapigapiga picha hapa kwa sababu gani, nitakumaliza mimi, alaa”.



Katika hatua ya mtuhumiwa akisaidia na askari kutaka kumpiga mwandishi, mwendesha mashtaka aliingilia kati na kuwataka askari waache fujo kwa kuwa mwandishi huyo hakuvunja sheria jambo lililowasababisha baadhi ya asjkari waliokuwepo hapo kutoka katika chumba cha mahakama wakiwa katika hali ya aibu.



“Waandishi wanaujua utaratibu wao, hebu mwacheni na yeye anafanya kazi katika nafasi yake. Muda wao wakupiga picha wanaufahamu hebu waacheni waandishi wawe huru, ni haki yao” alisema Maganda.

 

Mwangosi aliuawa kwa bomu Septemba 2 mwaka jana katika kijiji cha Nyololo Wilaya ya Mufindi alipokuwa akiwajibika kwa kazi za kihabari wakati wa ufunguzi wa matawi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).


No comments:

Post a Comment