Serikali
imeombwa kuweka zoezi la kila mwaka la uandikishaji wa vitambulisho vya wapiga
kura, kufuatia idadi kubwa ya watu Nchini hususani vijana kushindwa kujitokeza
katika zoezi la upigaji kura pindi linapotokea.
Haya
yalijitokeza jana wakati Mbunge viti maalum Chiku Abwao (CHADEMA), wakati wa
zoezi la kuunda kikundi cha TUJIJENGE cha wanawake wajasiliamali katika kata ya
Mwangata Mkoani Iringa, ambapo baadhi ya wanawake hao walidai kuwa, watanzania
wengi hawana vitambulisho vya kupigia kura kutokana na baadhi yao kupoteza na
wengine kufikisha umri wa miaka 18 hivyo kuwa na haki ya kumiliki kitambulisho
hicho kwaajili ya kumchagua kiongozi wanayemuhitaji.
Mmoja
wa wanawake hao katika kikundi hicho Rehema Mbetwa, alimuomba Mh. Chiku
kulifanyia kazi suala la vitambulisho, ili kuifanya Nchi ya Tanzania kuwa
na Demokrasia ya kweli kwa kumfanya kila mwananchi mwenye sifa ya kumiliki
kitambulisho hicho kukipata na kuwa na haki ya kumchagua kiaongozi anayemfaa.
“Hata
kama viongozi wetu watakuwa wanapiga kelele watu wajitokeze kupiga kura, endapo
watu watakuwa hawa vitambulisho vya kupigia kura haitasaidia kitu chochote”,
alisema Mbetwa.
Hata
hivyo Mbunge huyo alikiri kuwepo kwa changamoto hiyo na kudai kuwa endapo Serikali
ingekuwa inajali demokrasia, suala la upatikanaji wa vitambulisho lingekuwa ni
la kila mwaka, ili kuhakikisha kila Mtanzania anapata haki ya kuchagua ama
kuchaguliwa.
Mbunge
huyo alidai kuwa Suala la upatikanaji wa vitambulisho vya kupigia kura halijafanywa
kuwa la kila mwaka kwa maslahi ya kisiasa.
“Kwasababu
kunawakati vijana wengi walikuwa hawajali sana
masuala ya kupiga kura, wakapoteza vitambulisho vyao huku wengine walirubuniwa
na baadhi ya viongozi mbalimbali wakauza vitambulisho vyao, ndo maana sasahivi
chaguzi nyingi za marudio unakuta CCM walishinda kwa kishindo kikubwa kutokana
na wenye vitambulisho vya kupigia kura sasa hivi ni wazee ambao wapo CCM, huku
vijana wengi ambao ni wapinzani hawana vitambulisho.
Aliahidi
kulifuatilia suala hilo la vitambulisho ili liwe
endelevu kwa kila mwaka, na kudai kuwa endapo hawatalipitisha suala hilo CHADEMA itatumia
nguvu ya umma kudai haki hiyo.
Licha
ya changamoto ya vitambulisho ,Mh. Abwao aliongeza kuwa, kumekuwa na tabia ya
baadhi ya viongozi wa vyama vya kisiasa kuwabeba wapiga kura wakati wa kampeni za uchaguzi na
kuwapatia vitenge na kofia na kasha kupotea, badala ya kubuni mbinu endelevu za
kubadilisha maisha ya mtanzania.
“Kumekuwa na tabia ya wanasiasa kuwabeba wapiga kura na kugawa kanga, kofia na kutoa pesa bila kuwawezesha ili muweze kujitegemea lakini mimi natekeleza ilani ya Chama cha Demokrasia ya Maendeleo kuwawezesha wanawake wenzangu ili muweze kuboresha maisha yenu kuacha tabia ya utegemezi” alisema Abwao.
Alisema matatizo mengi yanapojitokeza wanaopata taabu ni wanawakejambo ambalo limekuwa mzigo mzito kwa sababu ya umaskini.
“Matatizo mengi ya umasikini yanatukumba sisi wanawake, umaskini
unatufanya tuwe watumwa na wanyonge kwa kuwa tunakuwa hatuna kitukinachoweza kutusaidia kutatua matatizo yanayotupata lakini tukiwatunajiweza kiuchumi, tunakuwa tayari kuyatatua matatizo hayo” alisema Abwao.
Alisema adui mkubwa wa wanawake ni umaskini na unyonge ambao unamfanya mtu kufa upesi kwa sababu ya kufikiri bila kupata ufumbuzi.
“Unyonge unatufanya kufa upesi kwa sababu ya mawazo. Adui yetu mkubwa wa wanawake ni umasikini. Tusikubali umasikini hata kidogo” alisema.
No comments:
Post a Comment