masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Wednesday, January 9, 2013

Mgunge kuongoza usafi Iringa

Hili ni moja ya dampo ambalo limetelekezwa na uchafu katika maeneo ya msikitini Kihesa katika Manispaa ya Iringa.
MBUNGE wa Jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA) anatarajia kuongoza wakazi wa mji huo katika operesheni ya siku mbili ya usafi katika Manispaa hiyo yenye ikiwa mpango kabambe wa kuuweka mji katika hali ya usafi.
Manispa hiyo kwa sasa inakabiliwa na hali ya uchafu kupindukia kutokana na kuibuka kwa madampo mengi ya kutupa taka yasiyo rasimi yanayotokana na uwezo mdogo wa Halmashauri kuwa na mpango wa kuuweka mji safi.
Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake leo Msigwa amesema ameliona tatizo hilo na tayari imewaomba msaada wadau mbalimbali waliojitolea magari, fedha na wengine wakidai watajitolea nguvu zao katika kufanikisha kazi hiyo.
“Manispaa inagari moja la kusomba takata, gari hilo limeshindwa kusombaa uchafu kutokana na kiwango kikubwa cha uchafu kinachozalishwa ndani ya Manispaa hii, hajuna sababu ya kumlaaumu mtu hii ni kazi ya kijamii,ombi langu ni kwa wananchi wote tujitokeza kwa wingi kesho kushirikiana na vijana waliokubali kujitolea kusafisha mji wa Iringa” amesema Msigwa.
Amesema suala la usafi wa mazingira halina uhusiana na chama chochoite cha siasa kwa kuwa athari zitokanazo na uchafu yakiwamo magonjw aya mulipuko hayawezi kuchagua watu kutokana na itikadi za vyama vya siasa.
“Uchafua ni hatari kwa wakazi wa Iringa hususani kipindi hiki cha mvua,kwani ni chanzo cha magonjwa ya lipuko na kipindupindu, magongwa ambayo yakitokea hayatachagua mtu kwa msingi wa itikadi ya chama chake cha siasa, hayawezi kuangakia mimi Chadema na Yule CCM” amesema Msigwa na kuongeza.
Amesema katika kufanikisha hilo tayari watu mbalimbali wamejitokeza kwa wingi baadhi yao wamejitolea gari zao kutumika kusomba takata,wengine wametoa fedha na baadhi ya vijana wameahidi kujitolea nguvu zao.
“Ombi langu kwenu ni kwamba ikiwa mtakuta vijana wakifanya kazi ya usafi wa mazingira kesho msiwapate wasaidieni ili kw apamoja tuwezi kufanikiw akuweka mji wetu katika hali ya usafi,siku za nyuma Manispaa ya Iringa ilikuw amiongoni mwa miji iliyoongoza kwa usafi Tanzania lakini kwa sasa umetupwa mbali nah ii sijui sababu yake ninini”alisema Msigwa na Kuongeza:
“Na huu si wakati wa kujadili kutafuta nani kasababisha bali ni wakati wa kushirikiana kuweka mji katika hali ya usafi na ndipo tuanza kuona wahusika wanasitahili kufanya nini” amesema.

No comments:

Post a Comment