masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Saturday, January 5, 2013

Tundu Lissu amuonya JK kuhusu Katiba Mpya


Na Happiness Elias, Iringa

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kimemtaka Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dokta Jakaya Mrisho Kikwete kueleza amepata wapi mamlaka ya kuisemea tume ya katiba kufuatia tamko lake alilotoa usiku wa kuamkia mwaka mpya 2013, juu ya maendeleo ya mchakato wa katiba mpya.

Akiongea katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Mwembetogwa Manispaa Iringa Januari 3 mwaka huu katika viwanja vya Mwembetogwa, Mbunge wa Singida Mashariki Mh.Tindu lissu alisema kuwa, Rais anatakiwa kueleza amepata wapi mamlaka ya kupanga ratiba juu ya katiba mpya itapatikana na kwa taratibu zipi.

Lissu alisema kuwa kwavile sheria inasema, Rais atajua maendeleo ya mchakato wa katiba endapo atapelekewa ripoti kutoka tume ya katiba, hivyo CHADEMA imemtaka Rais kueleza amejua lini, na nani amemuambia kwamba tume itamaliza kazi yake itakapofika mwezi Julai.

“Kama hana majibu ya maswali hayo, tunataka mwenyekiti wa tume ya katiba Jaji Joseph Warioba atuambie kwa nini Rais anazungumza mambo hayo, atuambie nani miongoni mwa wajumbe wa tume ambaye anapeleka maneno hayo Ikulu na atuambie tupate hizi taarifa kabla ya Januari 14 mwaka huu, kwani Januari 14 tutaanza kamati za bunge” alisema Lissu.

Kwa muujibu wa sheria yamabadiliko ya katiba tume inatakiwa kufanya kazi kwa miezi 18 ambapo mpaka sasa tume hiyo inamiezi saba tangu ianze kazi na ingetarajiwa kumaliza kazi yake Desemba 1 mwaka huu.

Rais alisema kwamba kazi ya tume ya katiba ya kuandaa rasimu ya katiba mpya itakamilika Mei 5 mwaka huu ambapo tume hiyo itamaliza kazi yake, pia alisema kuwa baada ya mwezi Mei tume ya katiba itaanzisha mabaraza ya katiba yakayojadili rasimu ya katiba mpya kazi itakayofanyika kati ya mwezi Juni hadi Agusti mwaka huu na baada ya hapo bunge maalumu la katiba litakutana mwezi Novemba mwaka huu kuipitisha katiba mpya.

Kutokana na maelezo ya Rais Kikwete kuhusiana na mchakato wa katiba alisema kuwa, kama kila kitu kitaenda kama wanavyotarajia katiba mpya itapatikana 2014 nchi itakapofikisha miaka 50 ya muungano.

“Sasa ndugu zangu hayo ni maneno ya Rais kuhusiana na mchakato wa katiba, hoja yangu ni kwamba, Rais Kikwete na Serikali yake na Chama chake wanahujumu utaratibu wa kupata katiba mpya, hali itakayosababisha Watanzania kupata katiba mpya kwa jina huku ikiwa na mambo yale yale ya kumkandamiza Mtanzania”

Alisema kuwa Tume ilianza kazi rasmi Juni 1 2012 ambapo kuanzia kipindi mambo yote juu ya tume katiba yamekuwa yakizungumzwa hadharani na mwenyekiti wa tume hiyo Jaji Warioba.
Jaji Warioba ndiye msemaji wa Tume ya mabadiliko ya katiba na ndiye anayepaswa  aeleze ratiba ya tume ikoje, na kwa muujibu wa sheria hiyo, mtu pekee anayeweza kutuambia kazi ya mchakato wa katiba itaisha lini ni Jaji Warioba pekee.

“Sijaona mahali popote ambapo sheria hii inatamka kwamba Jakaya Mrisho Kikwete amekuwa msemaji wa tume ya katiba. Sijaona mahali pameandwikwa Waziri mkuu Mizengo Pinda au Mawaziri wengine wa Kikwete au mwanashiria  mkuu wake ni wasemaji wa Tume. Wanaotakiwa kutuambia kinaendelea gani ni tume ya mabadiliko ya katiba chini ya Mwenyekiti wake Jaji Warioba na sio Rais Kikwete”

Alisema kuwa kwa muujibu wa sharia kifungu cha 8(3) kinachosema kuwa Tume itakamilisha kazi yake ndani ya kipindi kisichozidi miezi 18 kuanzia kuanzia tarehe ya kuanza kazi.

Kutokana na sheria hiyo, tume ya mchakato wa katiba ilianza Juni 1 2012 hivyo inapaswa kumaliza kazi Desemba 1 2013 na sio mwezi Mei 2013 kama alivyosema Rais Kikwete, na kudai kuwa huo ni mwanzo wa utaratibu wa kuchakachua mchakato huo.

Pamoja na urais wake, hana mamlaka ya kuzungumzia chochote juu ya kazi ya tume kabla tume haijamaliza kazi yake na kumkabidhi ripoti. sheria hii ya mabadiliko ya katiba kifungu cha 20(1) inasema kwamba, baada ya kukamilisha kazi yake tume itawakalisha ripoti kwa Rais Kikwete na Rais wa Zanzibar, ataijua ripoti pale tume itakapomaliza kazi yake na kumpelekea.

“Hii ya kusema atamaliza mwezi Mei ameitoa wapi? Nani amempelekea taarifa hizo? Kwenye sheria hii hakuna maali popote ambapo tume au mtu mwingine yeyote anaruhusiwa kumpelekea Rais taarifa yeyote kabla ya kazi ya tume kukamilika”

Aliongeza kuwa,Rais kuingilia kazi ya tume anavunjwa sheria ya mabadiliko ya katiba kutokana na kifungu cha 10 kinachosema kuwa tume itakuwa na mamlaka na uhuru kwa kadri itakavyokuwa muhimu kwaajili ya utekelezaji wa majukumu na mamlaka yake chini ya sheria hii na haitaingiliwa na mtu au mamlaka yeyote.

Alihoji yakuwa Kikwete atakuwa na makusudi gani ya kuhakikisha tume inamaliza kazi yake kabla ya muda ambao sheria imeuweka.

Aidha alisema kuwa kutokana na kifungu cha sheria cha 20(2), baada ya ripoti kupelekwa Rais, Rais anatakiwa ndani ya siku 31 atoe tangazo katika gazeti la Serikali litakaloitisha bunge la katiba juu tarehe na mahali ambapo bunge la katiba litakaa.

“Siku ya mkesha mwaka mpya Rais Kikwete  bado hajakabidhiwa ripoti, haya maneno aliyosema bunge litakaa Novemba 2013 aliyatoa wapi, ameyapata wapi? Kwa mamlaka ipi? Kwa sheria ipi? Hayo yote ni maandalizi ya kuchakachua zoezi la katiba mpya”

No comments:

Post a Comment