masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, January 22, 2013

Mimba mashuleni zikomeshwe

Mkurugenzi mtendaji wa TCDA Jackson Kiyeyeu akiwa ofisini kwake wakati wa mahojiano na mtandao huu.


Kufuatia tatizo sugu la mimba kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari Mkoani Iringa, Tanganyika Centre Development and Advocacy (TCDA) wameanzisha mkakati wa kumaliza tatizo hilo Mkoani humo.

Akizungumza na mtandao huu ofisini kwake leo Mkurugenzi mtendaji wa TCDA Jackson Kiyeyeu alisema kuwa, wameamua kushughulikia suala la mimba mashuleni kutokana na tatizo hilo kuendelea kukua kwa kasi licha ya kuwepo kwa sheria ya kuwabana wale ambao watapatika na hatia kama hiyo.

Amedai kuwa, sababu kubwa inayochangia kuendelea kwa tatizo la mimba mashuleni  ni kunatokana na vijana wengi kukosa elimu ya afya na uzazi.

“Vijana wengi wanashindwa kufikia malengo kwa sababu hawana elimu ya afya na uzazi ndiyo maana tatizo la mimba mashuleni linaendelea kuwa sugu na kuonekana kama ni kitu cha kawaida. Kwa hiyo tumeona tuanze kupambana na hili kwa kutumia njia mbalimbali ili tuweze kulimaliza kabisa” amesema Kiyeyeu.

Amesema zipo sababu nyingi zinazochangia suala la mimba kwa wanafunzi mashuleni ambapo wakianza kuzifanyaia kazi zinaweza kupunguza tatizo hilo kama siyo kumaliza kabisa.

Amefafanua njia zitakazotumika,kuwa ni pamoja na kuishauri familia moja kuthamini motto wa familia nyingine na kuchukulia kama motto wake pamoja na kutoa elimu kwa vijana juu ya changamoto za ujanani.

“Tutatumia njia mbalimbali katika pambano hili. Tutatoa elimu ya afya na uzazi kwa vijana, tutaunda vikundi vya vijana na kuvitumia katika kwa ajili ya kuzungumzia changamoto za ujana, tutatumia michezo kama njia moja wapo ikiwa ni pamoja na kugawa mipira katika vikundi hivyo pamoja na kuishirikisha jamii katika suala zima la malezi ili kila mtu amuone mtoto wa mwenzake kama mtoto wake” amesema.

Alisema jamii ina mwamko mdogo katika kushiriki suala la malezi huku baadhi ya watu kuendelea kuwarubuni watoto wa wenzao na kuwakatisha masomo.

“Watu wengine hawaheshimu watoto wa wenzao. Wanafunzi wengi wanaokatishwa masomo, wahusika ni watu wazima ambao tungetegemea wawe walezi wazuri na mfano mzuri wa mwenendo wa tabia lakini wamegeuka kuwa ndiyo watu wa kuogopwa” amesema.

Hata hivyo amesema kumekuwepo na ushirikiano duni kati ya wazazi na waalimu hali inayosababisha pengo kubwa la utekelezaji kwa vitendo katika suala zima la maezi na elimu.

“Kumekuwepo na tatizo la kutegeana malezi kati ya wazazi na waalimu. Mwalimu anabaki akilaumu kuwa wazazi wanawafundisha watoto tabia mbaya huku mzazi naye akimlaumu mwalimu kuwa hawajibiki ipasavyo” amesema.

Hata hivyo alisema pamoja na lawama kwa upande wa walimu na wazazi, baadhi ya waalimu wamekuwa siyo waadilifu na kutumia nafasi walizo nazo kwa kuwakwamisha wanafunzi wao.

“Baadhi ya waalimu siyo waadilifu has asana walimu wa kizazi kipya wanatumia nafasi zao kwa kurudisha maendeleo ya wanafunzi. Badala ya kufundisha kile anachotakiwa kumfundisha mwanafunzi, yeye anaanza mahusiano mengine kabisa. Tunataka ifike mahali hiyo tabia ikaisha kabisa” amesema.

Sambamba na waalimu hao, amesema wapo baadhi ya maafisa watendaji wa vijiji, mitaa na wa kata kutumia tatizo la mimba mashuleni kama njia ya kujipatia fedha.

“Kuna baadhi ya maafisa watendaji wamekuwa ni chanzo kikubwa cha tatizo hilo kwa sababu wanafurahia wanafunzi wanapopata ujauzito na kutumia mwanaya huo kwa kujipatia fedha. Wanaamua kuwaita wahusika na kutaka wawape fedha ili suala lisiweze kufikishwa kwenye vyombo vya sheria ndiyo maana watu wanaendelea kufanya hivyo wakijua kuwa watakapo patikana wanamalizana kiaina” amesema.

Utafiti uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana katika Manispaa ya Iringa pekee unaonesha kwa mwaka jana wanafunzi 34 walikatishwa masomo kwa sababu ya ujauzito.

Shule 9 za sekodari zilizofanyiwa uchunguzi, ziliweza kubainika kuwa na mimba 30 huku shule ya sekondari ya Mkwawa pekee yake ikipatikana na mimba 4 na shule za msingi 4 zilizofanyiwa uchunguzi zilipatikana na mimba 4.

No comments:

Post a Comment