masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Saturday, January 19, 2013

Umoja wa wanafunzi wa vyuo vikuu Iringa waiingia mzigoni

P1040530.JPG
P1040532.JPG

Umoja wa wanafuzi wa vyuo vikukuu katika Manispaa ya Iringa wameendele na zoezi la kufanya usafi katika Manispaa kama moja ya ushiriki wao katika masuala ya kijamii.

Licha ya kuonesha umoja wao katika maeneo mbalimbali bado muamko wa viongozi wa mitaa pamoja na madiwani wa kata husika wameonekana kutopendezwa na na masuala hayo kwa kile kinachoonekana kutoshiriki na kuahamasicha wananchi kuungana na watu mbalimbali.


Rose Mayemba ambaye ni mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA katika tawi la Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCO) mlipuko wa magonjwa mbalimbali hauchagui itikadi za vyama na waathirika ni mtu yo yote bila kujali cheo na chama chake.


“Suala usafi linamlenga kila mtu bila kujali itikadi za siasa. Magonjwa yanapotokea hayawezi kuchagua siasa au itikadi. Watu wanaoingiza itikadi ya vyama katika masuala ya afya wana mawazo fivyu” alisema.


Halmashari ya Iringa inapaswa kuangalia upya na kuzuia ujenzi holela wa nyumba ili kuhakikisha mazingira yanakuwa safi na kuendeleza utamaduni wa kuhifadhi mazingira.


“Halmashaur inatakiwa kuzuia ujenzi holela katika maeneo ya milima na badala yake maeneo hayo yapandwe miti. Mimi ningefikiri sehemu za milimani tungepanda miti ili kuendeleza mpango wa taifa kuhifadhi mazingira ili kulinga hali ya hewa kuwa safi lakini tunapojenga huko tunaendelea kuyaharibu” alisema.


Vitus Rupeche mwanafunzi wa Chuo Kikuu kishiriki cha Tumaini alisema watu wanaojiita wasomi na kuishi sehemu chafu ni kuidharirisha elimu.


“Wasomi hawawezi kuishi sehemu chafu. Hivyo sisi wanafunzi tunatambua kuwa tupo katika jamii kwahi tunaungana na jamii katika masuala ya ufasi kwa sababu ni jukumu letu kuhamasisha” alisema Rupeche.


Hata hivyo ameonesha masikitiko yake kuona viongozi wa mitaa pamoja na madiwani wa sehemu husika hawana muamko wa kushirikiana na wadau mbalimbali wa usafi katika kuyaweka mazingira yao safi.


“Kinachonisikitisha hapa ni pale ninapoona viongozi wa maeneo husika hawaoini umuhimu wa ufasi katika maeneo haya. Tutaendelea na itikadio zetu mpaka lini katika masuala haya ya kijamii? Inasikitisha sana” alisema na kuhoji.


Wakati huo huo Hilda Mbinda mwanafunzi wa RUCO alisema kushiri kwa viongozi hao ni kushindwa kufikiri na kujua maana ya usafi.


“Nitaendelea kuwashangaa hawa wanaoitwa viongozi. Kushindwa kushiriki katika masuala kama haya kunaonesha ni jinsi gani hawana fikra na kutoelewa maana ya usafi” alisema.


Naye Olime Mwakilembe alisema vijana wana uwezo mkubwa katika maendeleo na hivyo kuwataka wasiwe nyuma kutumia nguvu katika kupiga hatua za kimaendeleo.


“Sisi vijana tunaweza ndiyo maana tumeamua kutumia nguvu zetu katika masuala. Vijana tunaomba tushirikiane kwa pamoja katika ujenzi wa taifa letu. Tusikubali kuvutwa na watu wasiopenda maendeleo eti kwa itikadi za vyama” alisema Mwakilembe.


Wanafunzi hao walianza kwa kupanda miti katika maeneo ya viwanja vya bustani ya Manispaa maarufu kwa jina la (garden) na baadaye kufanya usafi katika maeneo ya makaburi ya Mlandege.

No comments:

Post a Comment