![]() |
| Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Peter Msigwa akiwahutubiwa wakazi wa Manispaa ya Iringa katika viwanja vya Mwembetogwa. |
![]() |
| Mbunge wa Musoma mjini Vicent Nyerere akiwahutubia wakazi wa Manispaa ya Iringa katika viwanja vya Mwembetogwa. |
![]() |
| Mamia ya wakazi wa Manispaa ya Iringa wakimsikiliza Mbunge wa Musoma mjini Vicent Nyerere katika viwanja vya Mwembetogwa. |
Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeahidi kufanya maandamano nchi
nzima endapo serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) watazima simu
wanazoziita feki pamoja na runinga, Januari 1, 2013 kwa sababu ya
teknolojia ya digitali (Joerg: hakuna uhusiano kati ya simu na mfumo wa
digitali! Irekebishwe!)
Akiongea
jana Jumatano, tarehe 19 mwezi huu, katika mkutano wa chama hicho
uliofanyika katika kiwanja cha Mwembetogwa, Iringa Manispaa, Mkoani
Iringa Mbunge wa jimbo la Musoma mjini Mhe. Vincent Nyerere alisema
kuwa, serikali ya Chama cha Mapinduzi inadhamiria kumkandamiza (Joerg:
Nadhani ni maneno khali sana...) Mtanzania wa hali ya chini.
“Nawaambia
wakizima simu na TV tutaingia barabarani. Ingekuwa mimi ndio mwenye
Serikali na Msigwa na Dokta Slaa na wengine, tungefanya hivi; Marufuku
kuingiza simu feki ili zilizopo zitumike mpaka zioze zenyewe, lakini sio
kwa kuzima simu wa runinga bali kuwapa wananchi taarifa wasinunue simu
feki“, alisema Nyerere.
Aliongeza
kuwa simu hizo hazitengenezwi nchini bali hutoka nje ya nchi, lakini
Serikali imeendelea kusisitiza juu ya wazo lake la kupiga marufuku simu
feki, huku yenyewe ikiendelea kuziingiza nchini.
“Hizi
simu hazitengenezwi hapa zinatoka nje, huingia nchini aidha kwa kupitia
uwanjwa wa ndege au mpakani ambapo serikali yote ipo pale wakiwemo
polisi, TRA, usalama wa taifa wapo. Hata hivi tunavyoongea kuna simu za
kichina zinapitishwa kuingia Tanzania”
Aliongeza
“Haiwezekani simu bado zipo sokoni, watanzania wote hawajapata habari,
wanaendelea kununua na zinawasaidia halafu serikali inataka kunazima. Ndiyo maana nikimwona mtu amevaa nguo ya CCM namshangaa sana”
Wakati
huo huo CHADEMA kimeahidi kufanya jitihada ya kudai twiga
waliosafirishwa nje ya nchi huku wakidai kuwa waliochukua twiga hao
waadhibiwe.
“Waziri
kivuli wa maliasili na utalii, tunaomba twiga wetu warudi, hatutaki
fedha zao. Hatuhitaji kitu kingine zaidi ya kurudishiwa Twiga, wazungu
waje na sio kuwapelekea“, alisema Nyerere.
“Waliochukua
twiga waadhibiwe. Sitaki kuamini kwamba ni Maige pekeyake alijipanga,
akaenda porini, akakamata twiga, akafunga, akabeba akapeleka kwenye
ndege. Wote waliokwenda kufunga twiga hao, walioidhinisha, wote
wachukuliwe hatua”, alisema Nyerere.
Aidha
aliwataka wabunge nchini kuhakikisha ifikapo Julai 2013 Waziri Mkuu
anaeleza Mwenge unatumia shilingi ngapi kutembea nchini, nani anahoji
fedha hizo na bajeti yake inatoka wapi? Na kudai kuwa wanachi
hawataendelea kutoa michango ambayo haitolewi takwimu juu ya kiasi
kilichochangwa, matumizi na kiasi cha pesa kilizobaki.
“Taifa
lilipokuwa dogo mbio za Mwenge zilikuwa ni sawa tu, lakini sasahivi
miaka 50 ya Uhuru, mbio za Mwenge sasa basi. Mbio za Mwenge zipo
kwasababu Mkuu wa Mkoa,Mkuu wa Wilaya na wengine wanapiga dili na polisi
wanakaa nyuma kwenye defender wanasindikiza koroboi inawaka nchana”
alisema Mbunge huyo.
Hata
hivyo Nyerere alisema kuwa haoni sababuya kuwepo waziri wa viwanda
wakati nchi yenyewe haina hata kiwanda kwa kuwa hiyo ni moja ya matumizi
mabaya ya fedha za ewalipa kodi.
“Kuna
sababu gani ya kumpa waziri asimamie viwanda wakati hatuna viwanda?
Mnaongezea ukubwa wa serikali na kupoteza fedha za walipa kodi pasipo
sababu yo yote” alisema.
Aidha
alisemsa watu wanapokuwa na shida ya maji, viongozi wanachukua pesa za
walipa kodi na kununulia magari na kuwaacha wananchi katika matatizo.
“Watu
wanashida ya maji lakini tumeletewa magari kila kona ya maendeleo ya ya
programau ya maji. Je, watu wanashida ya mari au wanashida ya maji?”
alisema.
Alisema maendeleo siyo imani inayozungumzwa kwa maneno bali ni vitendo na utekelezaji.
“Maendeleo
sio imani ambayo unasema utaeleza kwa maneno na kuwaaminisha watu.
Maendeleo yanatakiwa kutekeleza kwa vitendo” alisema.
Wakati
huo huo Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa
alizungumzia, baadhi ya viongozi wa CCM ambao wamekuwa wakifanya ujanja
wa kuwapigia simu wafuasi wa CHADEMA kwa lengo la kuwanunua, huku baadhi
yao wakionesha kukubali.
“Ujanja
wa CCM wanajua kabisa kama wananchi hamuwataki, njia pekee wanayotumia
mpaka sasa ni ile ile ya kujaribu kuwarubuni watu, hivi ninavyozungumza
pale ofini kwangu wanachama makini wanapigiwa simu sana na
viongozi wa CCM wakitaka kuwanunua huku baadhi yao wakionesha dalili za
kununuliwa. Wale wanaopenda kwenda ni bora wakaenda mapema” alisema
Msigwa.



No comments:
Post a Comment