masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Tuesday, December 4, 2012

KITONGA BONANZA LAFANIKIWAi





Ilula stars wakiondoka na gari baada ya kupokea zawadi ya ushindi kiwanjani hapo kurudi nymbani kwao Ilula.
Mchezo wa bonanza uliochezwa jana katika kiwanja cha Mahenge kata ya Mahenge Wilaya ya Kilolo katika Mkoa wa Iringa, Ilula stars waliweza kuibuka na ushindi katika nafasi ya mshindi wa kwanza na kujichukulia zawadi nono.

Bonanza hiyo iliyoandaliwa na Stacom Kitonga Hotel ilishirikisha timu 8 za vijana kwa lengo la kuinua vipaji vya vijana ambapo vinaja hao waliibuka na zawadi mbalimbali.

Ilula stars ilweza kuibuka na ushindi huo baada ya kuichabanga Mgowelo mabao 2-1 katika nafasi ya nusu fainali mabao yaliyofungwa na Amani Myovela na Nansuli Mbululo yaliyopatikana katika dakika ya 16 na 22 katika kipindi cha kwanza huku Mgowelo wakiambulia goli moja lilofungwa na Fanye Ng’eve katika dakika ya 10 katika kipindi cha pili.

Katika hatua hiyo ya nusu fainali, Magana na Mahenge walishindwa kuoneshana ubabe ndani ya dakika 90 za mchezo na kulazimishana sare ya bila kufungana hali iliyolazimika kupigwa mikwaju ya penati na kuwezesha timu ya Mahenge kuingia katika fainali kwa mabao 6-5.

Katika nafasi ya kutafuta mshindi wa tatu, timu ya Magana ilitolewa na Mgowelo kwa goli 1-0 lililofungwa na Gawe Masambuli ambalo lilipatikana kwa njia ya penati ndani ya daki za mchezo.

Timu ya Mahenge ilishindwa kutamba mbele ya Ilula stars katika fainali baada ya kulambwa bao 1-0 na kufanikiwa kuingia katika nafasi ya mshindi wa pili.

Alikuwa Salim Kaywanga wa Ilula stars aliyeipatia timu yake ushindi baada ya kujitisha kichwani mpira wa kona iliyopigwa na William Chang’a katika dakika ya 19 katika kipindi cha kwanza.

Katika ushindi huo Ilula stars ikashika nafasi ya mshindi wa kwanza na kujipatia zawadi ya pampu ya maji yenye thamani ya shilingi laki nne (400,000), Mahenge mshindi wa pili wakijipatia zawadi ya seti ya jezi na fadha tasilimu shilingi sabini elfu (70,000/= huku Mgowelo ikiwa mshindi wa tatu wakijipatia fedha tasilimi shilingi laki moja na ishirini elfu (120,000/=).

Jumla ya timu 8 zilizoshiriki katika bonanza hilo ni Nice Moab kutoka kijiji cha Mahenge, Mahenge Shooting Stars kutoka kijiji cha Mahenge, Home Boy’s kutoka Ruaha Mbuyuni na Black Stars Ruaha Mbuyuni.

Timu zingine ni Fire Store kutoka kijiji cha Msosa, Magana Sports kutoka kijiji cha Magana, Mgowelo kutoka kijiji cha Mgowelo na Ilula Stars kutoka Ilula.

Black Stars waliweza kujipatia fedha tasilimu shilingi hamsini elfu (50,000/=) kama timu bora huku mchezaji bora akiwa Juma Ismail kutoka timu ya Magana akijipatia fedha taslimu shilingi elfu kumi (10,000/=).

Gawe Masambuli kutoka timu ya Mgowelo alijipatia fedha taslimu shilingi elfu kumi (10,000/= kwa kuwa mfungaji bora huku olikipa bora akiwa Shafii Ngenzi wa timu ya Mahenge shooting stars akijipatia shilingi elfu kumi (10,000/=) wakati huo marefalii watatu wakikijipatia ishirini (20,000/=) kila mmoja.

Akizungumza na mtandao huu kwa niaba ya mwandaaji wa bonanza hilo Stacom Kitonga Hotel, Wallafrid Mgina alisema nia ya hoteli ya Kitona ni kuwaunganisha vijana katika upenda pamoja na kujenga mahusiano mazuri baina ya hoteli ya Kitona na wananchi.

“Sisi tunataka kuwaunganisha vijana katika upendo na kujenga mahusiano baina yetu na jamii ili iweze kutambua uwepo wetu na huduma tunazozitoa. Pia tunataka kile kidogo tunachokipata tusaidiane” alisema Mgina.

Mgina alisema pia anataka kuwakumbusha wafanyabiashara kuwa wananafasi kubwa katika kutoa michango yao kwa jamii inayowazunguka badala ya kusubiri kuombwa misaada tu.

“Vile vile tunataka kuwakumbusha wafanyabiashara kuwa wakati wakat ambao wanatakiwa kutoa ushirikiano na jamii ni pale wanapotoa sehemu yao badala ya kusubiri kuombwa” alisema.

Bonanza hilo limekuwa changamoto kubwa kwa viongozi mbalimbali wa serikali hasa wanasiasa kwa pale wanapokuwa wahamasishaji wa michezo bila kuwepo na utekelezaji.

Akizungumza katika mahojiano na mtandao huu, diwani wa viti maalumu wa kata ya Mahenge Sheila Ngailo alisema kuwa inabaki kuwa changamoto kwao katika kuandaa michezo kwa vitendo.

“Hii inabaki kuwa changamoto kwetu kwa kuwa tumekuwa wahamasishaji bila kufanya kwa vitendo. Kazi inabaki kwetu kama viongozi wa maeneo husika” alisema.

Ikiwa Bonanza hilo lilikuwa la kwanza katika kata hiyo, lilikuwa na mwitikio mzuri wa wachezaji na mashabiki mbalimbali

No comments:

Post a Comment