masuguru

Tangazo la cheti

Tangazo la cheti
tangazo

KLERUU

KLERUU
KLERUU

CAPRICORN

CAPRICORN

Ibada

Ibada

Monday, December 24, 2012

Jamii ya Wahadzabe kikwazo cha sensa


JAMII ya wawindaji na waokota matunda wa kabila la Wahadzabe waliopo katika Wilaya ya Karatu mkoani Arusha ni changamoto kubwa iliyoligubika zoezi la uandikishaji wa sensa ya watu na makazi iliyofanyika Agosti 26 baada ya jamii hiyo kutoa masharti ya kupatiwa nyama ili wahesabiwe.

Hayo yalisema jana na Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk. Albina Chuwa wakati wa kufunga mkutano wa tano wa baraza la wafanyakazi wa ofisi hiyo uliofanyika kwa siku mbili mjini hapa.

“Katika mambo ambayo tumejifunza wakati wa zoezi la kitaifa la uandikishaji wa sensa ya watu na makazi iliyofanyika Agosti 26 mwaka huu ni wenzetu Wahadzabe namna ambavyo walitoa masharti  kwa serikali wapatiwe nyama na wakahesabiwa. Kwa kweli ilikuwa changamoto kubwa na tumejifunza mengi na kimsingi tunazifanyia kazi changamoto zilizojitokeza,”Alisema Chuwa.

Jamii ya Wahadzabe haijishughulishi na kazi za kilimo wala ufugaji na badala yake, wanategemea uwindaji na kuokota matunda kama njia kuu ya kujipatia chakula.

Desemba 31 mwaka huu, Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kutangaza matokeo ya sensa ya watu na makazi wakati atakapolihutubia taifa katika hotuba yake ya mwisho wa mwaka ambapo pamoja na mambo mengine, atatangaza idadi ya watanzania waliopo nchini hivi sasa.

Sensa ya watu na makazi ilifanyika kwa mara ya kwanza mwaka 1910, sensa nne za mwisho zilifanyika baada ya Uhuru, katika miaka ya 1967, 1978, 1988 na 2002.

Hata hivyo wakati taifa likisubiri kwa hamu kubwa taarifa hiyo ya Rais Kikwete, Tanzania inakadiriwa kuwa na idadi ya watu zaidi ya milioni 34 kutokana na sensa ya watu na makazi iliyofanyika kwa mara ya mwisho mwaka 2002.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayoub alisema kuwa umma unapaswa kuelimishwa kwamba matokeo yaliyopatikana katika zoezi la uandikishaji wa sensa ya watu na makazi ya mwaka huu yatatumika kuongeza ubora na kupanua wigo wa uzalishaji wa takwimu za msingi kama vile pato la taifa, mfumuko wa bei na takwimu za viashiria mbalimbali vya kijamii na kiuchumi.

No comments:

Post a Comment