| Mwezeshaji wa mafunzo ya uandishi wa habari za afya Dk. Ahmed Twaha akitoa mafunzo kwa waandishi |
| Katibu mtendaji wa IPC Frank Leonard akifungua mafunyo. |
| Washiriki wa mafunyo wakimsikiliza mwezeshaji |
WANAHABARI
wametakiwa kuandika habari za afya hususani juu ya magonjwa mbalimbali na
lishe, ili kuweza kuisaidia jamii kuachana na imani potofu zinazohusiana na
matibabu ya magojwa
Ushauri
huo ulitolewa na mtaalamu wa afya ya binadamu Dk. Ahmed Twaha muweyeshaji wa
mafunzo ya uandishi wa habari za afya kwa waandishi wa habari wa Mkoa wa Iringa
yalizoanza jana katika ukumbi wa maktaba ya Mkoa.
Dk. Twaha
alisema kuwa, habari za afza zikiandikwa mara kwa mara zitaiwezesha jamii kujua
namna ya kupata matibabu kwa ugonjwa husika unaosumbua kwa wakati huo.
‘Jamii
yetu inashindwa kujua nini maana ya afya kwa sababu habari nyingi haziwafikii.
Hii inatokana na ninyi wanahabari kutokuandika habari za afya mara kwa mara na
kusabaisha jamii iwe na imani potofu ya
kutegemea waganga wa jadi juu ya magonjwa yanayoweza kutibika hospitalini’
alisema Dk. Twaha.
Alisema habari
za afya katika jamii ni za muhimu katika uimarishaji wa uchumi katika Taifa
kwani nguvu kazi kubwa imekuwa ikipotea kwa sababu ya magonjwa mbalimbali
ambayo yanatibika.
‘Kushuka
kwa uchumi kuchangiwa kwa kiasi na kupotea kwa nguvu kazi ambayo kwa kiwango
kikubwa ni magonjwa yanayotibika. Kwa hiyo kwa nguvu yenu wanahabari mnaweza
kufichua magonjwa katika maeneo mbalimbali yanayoitesa jamii kwa kuamini kuwa
wamelogwa badala ya kwenda kupata matibabu kwa wataalamu wa afya’ alisema.
Dk. Twaha alisema kutokana na jamii
kukosa elimu sahihi ya afya wengi wamekuwa
wakipoteza maisha kwa kukosa
msaada wa kitabibu.
Akifungua mafunzo hayo, Katibu
mtendaji wa IPC Frank Leonard alisema mafunzo hayo ni mwendelezo wa
mafunzo mbali mbali ambayo umoja wa klabu za
waandishi wa habari Tanzania (UTPC) imekuwa ikiyatoa
kwa vilabu mbalimbali nchini ikiwemo IPC.
Alisema
mafunzo hayo yatasaidia ujuzi kwa wanahabari katika kuandika habari
za afya kwa kuzingatia ubora na taarifa sahihi katika habari zinazohusu
afya.
Leonard
alisema wengi wao wamekuwa wakiandika habari zinazohusu afya pasipo
kuwa na utaalam na kusabababisha jamii kutokujua masuala yanayohusu afya na
kutotilia maanani juu ya matibabu yake lakini kupitia mafunzo haya watakuwa na
ujuzi wa kuandika habari hizo kwa undani zaidi.
Mafunzo
hayo ya siku nne yaliyoanza hapo jana ambapo
yanatarajiwa kumalizika Novemba 22 mwaka huu, huku waandishi watapata fursa za
kutembelea katika hospitali ya Mkoa katika vitengo mbali mbali vya afya kujua
changamoto wanazokutana nazo hasa magonjwa makubwa yanayoitesa jamii.
No comments:
Post a Comment