| Damu ya marehemu Bathlomeo Nzigilwa iliyotiririka baada ya kujeruhiwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi. |
Aliyekuwa mlinzi wa Kanisa Katoliki Parokia ya
Kihesa Jimbo la Iringa Bathlomeo Nzigilwa anzikwa leo katika makaburi ya
Semtema ndani ya Manispaa ya Iringa.
Nzigilwa alivamiwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi
usiku wa kuamkia Novemba 15 mwaka huu na kumjeruhi vibaya na kufanikiwa kuvunja
milingo ya Kanisa na kuiba baadhi mali.
Nzigilwa alifariki dunia 24 Novemba katika Hospitali
ya Taifa ya Mhimbili alikopelekwa kutibiwa baada ya kutolewa katika hospitali
ya Mkoa wa Iringa.
No comments:
Post a Comment